Facebook

Sunday 29 March 2015

Huyu ndiye binadamu wa kwanza aliyepandikizwa Moyo wa binadamu aliyekufa.

Madaktari wa upasuaji huko Cambridgeshire wamefanya upandikizaji
wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa kutumia moyo mwengine
uliosimama kufanya kazi.

Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa watu waliokufa lakini ambao
myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka kwa mtu ambaye mapafu yake
na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.

Hospitali ya Papworth inasema kuwa mbinu hiyo huenda ikaongeza
idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa jina Huseyin Ulucan, mwenye
umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na shinikizo la moyo
mwaka 2008.

Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza kutembea na nilichoka sana,kwa
hakika siku na maisha mazuri.
Upandikizaji wa moyo
Lakini anasema kuwa amefurahishwa na kuimarika kwa afya yake
tangu upandikizaji huo.

Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila siku,na nimetembea hadi
haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha
miaka 12 iliopita nchini Uingereza.

Lakini mahitaji yanashinda myoyo iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine
hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla ya kiungo kupatikana.

0 comments:

Post a Comment