Facebook

Sunday 29 March 2015

Upagaji busu hadharani wapigwa marufuku India.

Kijiji kimoja nchini India kilichopo katika jimbo la kusini magharibi
kimepiga marufuku upigaji busu wa hadharani na tabia nyengine
mbaya.

Bunge la kijiji hicho kwa jina Salvador -de Mundo lililopo kilomita
maili nane kutoka kazkazini mwa mji mkuu wa Goa Panaji,lilipitisha
sheria hiyo kwa wingi likiwaonya watu wanaozuru eneo hilo dhidi ya
vitendo kama hivyo.

''Tumeidhinisha sheria hii kufuatia malalamishi kutoka kwa wakaazi
kuhusu wapenzi wanaopigana busu hadharani'',.Hii ndio hatua ya
kipekee ambayo itaweza kukabiliana na tatizo hilo'',naibu chifu wa
kiji hicho Reena Fernandes aliambia AFP.
Hatahivyo hakusema ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya wakiukaji
wa sheria hiyo.

0 comments:

Post a Comment