Facebook

Thursday 17 September 2015

David Busst amtabiria Shaw kurudi mapema uwanjani.

Mchezaji Luke Shaw anateseka baada ya kuvunjika mfupa mara mbili katika mguu wake wa kulia Jumanne usiku.
Alikuwa akiitumikia timu yake katika michuano ya Champions League kwa timu yake ya Manchester United dhidi ya PSV.

Mchezaji wa zamani wa Coventry, David Busst anaamini Luke Shaw atarudi uwanjani kabla ya kuisha msimu huu
Busst aliwahi kuvunjika dimbani Old Trafford mwaka 1996, katika mchezo dhidi ya Coventry na United ambapo alimaliza soka lake miezi michache baadae.

Taarifa zinasema mchezaji huyo anaweza kurudi uwanjani baada ya miezi sita.

Toa mtazamo wako baada ya kuvunjika kwa Shaw mguu wake!

0 comments:

Post a Comment