Facebook

Thursday 17 September 2015

Jennifer Hudson akolea kwa penzi la Mkenya.

Ni miaka sita sasa tangu wawili hawa wawe kwenye mahusiano huku wakijaliwa kupata mtoto wa kiume ambaye ana uri wa miaka mitano.

Pengine wengi walidhani muimbaji na muigizaji mwanadada Jennifer Hudson hatadumu kwenye penzi la mcheza miereka mwenye asili ya nchi ya Kenya David Otunga kutokana na mapenzi ya maisha ya kistaa kutokudumu lakini kwa upande wao mambo yanazidi kunyooka.

Inaripotiwa ili kuimarisha penzi lake, Jennifer Hudson hataki hata kumuachia na kuwa mbali na Baba mtoto wake huyo. Mapema jumatano wiki hii kamera za mapaparazi ziliwanasa wawili hao wakiwa pamoja kwenye mtoko tamasha la wiki ya mitindo na urembo huko marekani.

0 comments:

Post a Comment