Facebook

Thursday 17 September 2015

Huyu ndiye Mbuzi anayekunywa Chai ya Maziwa.

Mwandishi na mpiga picha Mohamed Jabra kutoka Gaalkayo, katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Somalia, eneo la Puntland, amesema baada ya mlo wa jioni jana, alikwenda kwenye mgahawa mmoja akiwa na rafiki yake na kuagiza vikombe viwili vya chai.

"Ghafla alitokea mbuzi na kutaka kunywa chai yangu," Mohamed alisema. "Nilijaribu kumzuia, lakini hakukubali, ikabidi nimuachie tu anywe chai yangu."

Amesema mbuzi huyo 'aligida' chai hiyo haraka haraka, licha ya kuwa ilikuwa ya moto.
"Ikabidi nijiliwaze kwamba, kwa kuwa chai yenyewe ilikuwa ya maziwa ya mbuzi, kwa hiyo alikuwa na haki ya kuing'ang'ania."

0 comments:

Post a Comment