Facebook

Saturday 26 September 2015

PROF KITILA MKUMBO:TADIP(TAASISI ILIYITOA UTAFITI JANA) NI N.G.O YA CHADEMA

Imebainika kuwa Zitto Kabwe alikuwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Development Initiative (TADIP) kabla hajaondoka chadema.

Kwa mujibu wa Prof. Kitila Mkumbo, "...TADIP is chadema's NGO. Zitto was once a Director"

Zitto wa CHADEMA amefanya kazi hiyo ndani ya taasisi hiyo, malengo yake yakiwa ni kutoa mtazamo chanya wa matokeo wakati wa uchaguzi au pia jambo lolote linalohusu chadema.

TADIP pia imekuwa inafadhiriwa na taasisi moja ya ujerumani, ambayo pia imekuwa inaifadhili CHADEMA.

Prof Mkumbo pia aliwahi kuwa mwanachama wa CHADEMA. Taasisi hiyo Jana imetokea matokeo ya maoni ya wananchi kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu. Matokeo yake yaliyotiliwa shaka, yalikuwa tofauti sana na taasisi zingine zote zilizofanya tafiti kama hizo.

0 comments:

Post a Comment