Facebook

Monday 21 September 2015

Mh.Lowassa alitikisa tena Jiji la Dar es Salaam.

Mgombea urais wa Chadema kupitia UKAWA Mh.Lowasa atikisa jijini Dar es Salaam.
Mgombea urais wa UKAWA Edward lowassa Katika mikutano mikubwa ya hadhara aliyoifanya kwa nyakati tofauti na kuhudhuliwa na maelfu ya wakazi wa jijini Dar es Salaam amesema serikali yake ya awamu ya tano itajikita katika kuhakikisha inaboresha maisha ya watanzania wanyonge ambao wameshindwa kunufaika na rasmili za nchi kwa miaka 50 iliyopita.

Lowassa ameomba Watanzania wametakiwa kutokukubali kuhadaika na ahadi zinazotolewa na baadhi wa wagombea katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu kwani wengi wao hawana dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment