Facebook

Thursday 17 September 2015

Maafisa wa kikosi cha ulinzi cha rais nchini Burkina Faso wametangaza kuvunja serikali ya mpito.

Maafisa wa kikosi cha ulinzi cha rais nchini Burkina Faso wametangaza kuvunja serikali ya mpito. Badala yake "Baraza la Kidemokrasia na Kitaifa" ndio litachukua udhibiti na kumaliza "utawala dhalimu", amesema afisa mmoja kupitia kituo cha TV cha taifa. Spika wa bunge wa kipindi cha mpito Cheriff Sy amesema hatua hiyo ni "mapinduzi dhahiri".

Kuna mapigano makali yanaendelea katika medani ya mapinduzi jijini humo. Siku ya Jumatano, kikosi cha rais kiliwakamata rais wa mpito na waziri mkuu. Walikuwa wakitarajiwa kukabidhi madaraka kwa serikali mpya Oktoba 11 baada ya uchaguzi. Rais aliyekaa madarakani kwa muda mrefu Blaise Compaore, aliondolewa madarakani mwaka jana kutokana na nguvu ya wananchi.

0 comments:

Post a Comment