Facebook

Thursday 17 September 2015

Jengo refu Afrika lazinduliwa Tanzania.


Jengo la PSPF Towers lililozinduliwa na Rais Kikwete hapo jana ni moja ya majengo machache marefu barani Afrika na ndiyo jengo refu zaidi LILILOKAMILIKA Afrika Mashariki na Kati, likiwa na urefu wa mita 147. Ujenzi wake ulitumia miaka minne tangu mwaka 2011 hadi 2015 na limegharimu shilingi bilioni 139.20 za Tanzania. Lina maeneo ya ofisi na nyumba za makazi 88. Pia katika jengo hili kuna sehemu ya Mgahawa, Mabenki, Bwawa la kuogelea, Sehemu za kufanyia mazoezi, Maegesho ya Magari na sehemu nyingine muhimu.

0 comments:

Post a Comment