Facebook

Thursday 24 September 2015

Magari yalioibwa Uingereza yapatikana Uganda

Wapelelezi waliokuwa wakilitafuta gari moja aina la Lexus lililoibwa mjini London nchini Uingereza wamelipata nchini Uganda.
Gari hilo lilikuwa na kifaa kinachoonyesha liliko.
Walipolipata nchini Uganda ,lilikuwa miongoni mwa magari 28 ya kifahari kutoka Uingereza yenye thamani ya zaidi ya pauni milioni moja,kulingana na gazeti la Metro nchini Uingereza.
Inadaiwa kuwa wezi hao walibadilisha mfumo wa kutumia funguo ya kuyawasha magari hayo.

0 comments:

Post a Comment