Facebook

Thursday 4 June 2015

Argentina waandamana kutetea wanawake

Maelfu ya watu wameandamana katika mji mkuu wa Argentine - Buenos Aires kupinga mateso dhidi ya mwanamke .
Maandamano hayo yamefuatia mfulurizo wa visa vya mauaji yaliyoshtua taifa hilo , yakiwemo yale ya mwalimu wa chekechea ambaye bwana yake alimkata koo mbele ya darasa lake .
Vyama vya wafanyakazi , vyama vya kisiasa na kanisa katoliki wameunga mkono maandamano hayo Argentina imepitisha sheria dhidi ya unyanyasaji wa nyumbani, lanini wanaharakati wanasema kuwa hazitekelezwi ipasavyo .
Maandamano ya watu wachache pia yamefnyika katika nchi jirani za Chile na Uruguay.

0 comments:

Post a Comment