Facebook

Thursday 4 June 2015

Barcelona yamkataza Figo kuvaa jezi yao


Luis Figo alikuwa mhimili wa Barcelona kabla ya kutimkia Real Madrid mwaka 2000
Luis Figo alikuwa mhimili wa Barcelona kabla ya kutimkia Real Madrid mwaka 2000
Barcelona wamemtaka Luis Figo kutowakilisha klabu yao katika mechi ya magwiji siku ya Ijumaa jijini Berlin.
Figo alikaa miaka mitano Nou Camp kabla ya kuhamia kwa mahasimu Real Madrid mwaka 2000 na alichaguliwa na UEFA kwenye timu zinazounda Juventus na Barcelona kuikabili timu ya Dunia XI.
Figo akiziba maskio baada ya kuzomewa na mashabiki wa Nou Camp kufuatia uhamisho wake Real Madrid
Figo akiziba maskio baada ya kuzomewa na mashabiki wa Nou Camp kufuatia uhamisho wake Real Madrid
Hata hivyo, Barcelona wameitaka UEFA kumuondoa kwenye kikosi chao baada ya maandamano ya mashabiki, ambao ni miaka 15 bado wana hasira nna uhamisho wake uliokuwa na utata.

0 comments:

Post a Comment