Facebook

Saturday 6 June 2015

Xavi kuondoka Barca kwa heshima.

Wakati Xavi Harnandez,35, anajiandaa na kustaafu rasmi baada ya kuitumikia Barcelona kwa miaka 17 ya maisha yake, swali je, atafanikiwa kuongeza kombe jingine hapo keshokutwa.

Barcelona inashuka dimbani mjini Berlin, Ujerumani kucheza fainaliya Ligi ya Mabingwa Ulayadhidi ya Juventus ya Italia.Utaona katika picha hiyo hapo juu, Xavi akiwa amezungukwa na makongwe 24 aliyowahi kubeba akiwa na Barcelona kwa miaka 17.

Hapo kuna makombe manane ya La Liga, matatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, mawili ya UEFA Super Cups, matatu ya Copa del Reys, sita ya Spanish Supercups na mawili ya Kombe la Dunia kwa klabu.
.JE! ATAWEZA KUBEBA UBINGWA WA 25 NDANI YA BARCA KABLA AJASEPA?

0 comments:

Post a Comment