Facebook

Thursday 4 June 2015

Zitto:Ccm isipomteua Mh.Benard Membe nitaishangaa.


Aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini ndugu Zitto Kabwe ametoa kauli nzito ambayo haijawahi kutolewa na kiongozi yeyote wa upinzani nchini.

Zitto alitoa kauli hiyo akiwa mkoani Kigoma kwenye maandalizi ya kujiandikisha na zoezi la uandikishaji katika daftari la kupigia kura.
Zitto aliwaambia wananchi wa Kigoma waliomuuliza juu ya mtazamo wake namna makundi yanavyoitafuna Ccm kwenye suala la urais kuwa mgombea pekee wa kuivusha nchi ni Bernard Membe.
"Membe ni kiongozi makini.Ana historia nzuri kiutendaji serikalini.Hata upinzani tunajua akiteuliwa yeye agombee kupitia Ccm itatusumbua sana" alisema Zitto.
Kauli ya Zitto imechukuliwa kwa uzito wa hali ya kipekee na watanzania wa ukanda wa magharibi.
Source:Mwananchi.

0 comments:

Post a Comment