Facebook

Wednesday 3 June 2015

Man United yamuwinda Dani Alves.

 
Kilabu ya Manchester United inaamini iko katika nafasi nzuri ya kumsajili Dani Alves kutoka Barcelona iwapo kocha Louis Van Gaal anataka kumsajili beki huyo wa kulia.
Alves atakuwa hana mkataba mwishoni mwa msimu huu na Barcelona iko tayari kumwachilia beki huyo wa miaka 32 kuondoka baada ya mechi ya fainali ya vilabu bingwa Ulaya dhidi ya Juventus siku ya jumamosi mjini Berlin.
Klabu ya PSG pia inamuania Alvez ijapokuwa kocha wake Laurent Blanc anaamini mchezaji huyo bado anataka kusalia Barcelona.
Lakini maoni ya Old Trafford ni kwamba Alvez hangependelea kujiunga na PSG.
Van Gaal anapanga kumsajili beki wa kulia.Licha ya umri wake mkubwa ukosefu wa fedha za uhamisho zinamfanya mchezaji huyo kuwa muhimu.
Mchezaji huyo wa Brazil anapokea kitita cha pauni 120,000 kwa wiki, fedha ambazo United inaweza kuzilipa bila kutoa jasho.

0 comments:

Post a Comment