Facebook

Monday, 1 June 2015

Ujumbe wa Rio Ferdinand baada ya kutundika jaruba.

yeye
Akiwa bado kwenye majonzi makubwa ya mkewe aliyefariki duniani mwanzoni mwa mwezi huu, beki wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England Rio Ferdinand ameweka wazi mikakati yake mipya katika mahojiano aliyoyafanya.
Mchezaji huyo ambaye kwa sasa ana miaka 36 ametangaza nia ya kustaafu soka baada ya klabu ya Queens Park Rangers kutangaza kumtema kwenye kikosi chake.
na mkewe
Rio Ferdinand akiwa na marehemu mkewe Rebecca
Alitangaza uamuzi wake katika mahojiano ya moja kwa moja na BT Sport, na aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter kuwashukuru waliomtakia kila la heri baada ya kifo cha mkewe, Rebecca aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani, ambaye wamezaa naye watoto watatu.
Ferdinand hakuacha kumsifia kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson kwamba ni mfano wa kuigwa kutokana na ujuzi wake.
Manchester United ilitoa Pauni Milioni 30 kumnunua Ferdinand Julai mwaka 2002 na kumfanya awe beki ghali katika historia ya soka ya Uingereza wakati akisajiliwa kutoka Leeds United.

Related Posts:

  • Madrid wafungua mazungumzo na Raheem Sterling.Real Madrid imefungua mazungumzo ya kumnyaka mchezaji Raheem Sterling kwa ada ya uhamisho wa Euro milioni 45.Mchezaji huyo machachali anataka kuondoka Liverpool na matajiri wa Hispania wapo tayari kukamilisha mpango wa ku… Read More
  • Walcott akataa kuzungumzia mkataba mpya ArsenalTheo Walcott hataki kuonyesha muelekeo wake ndani ya Arsenal ingawa mkataba wake umebakisha mwaka mmoja kuisha.Walcott alifunga katika fainali ya FA dhidi ya Aston Villa kwa ushindi wa 4 - 0.Mchezaji huyo ameviambia vyombo … Read More
  • Brendan Rodgers asalia Liverpool. Brendan Rodgers anabaki klabuni Liverpool baada ya mazungumzo mazuri na mwenyekiti wa timu hiyo Tom Werner. Mazungumzo hayo yame mbakisha Rodgers kuwa meneja wa Liverpool. Je! maamuzi ya kumbakisha Brendan Anfield, ikiwa t… Read More
  • Liverpool yamkosa mshambuliaji hatari LacazetteTimu ya Liverpool itashindwa kumsaini mchezji Alexandre Lacazette ,baada ya Rais wa timu ya Lyon Jean-Michel Aulas kusema mchezaji wake hatojiunga na Liverpool kufuatia timu hiyo ya Anfield kukosa nafasi ya kushiriki Cha… Read More
  • James Milner atua Liverpool.Kiungo James Milner anakamilisha uhamisho kwenda Liverpool akitokea timu Manchester City midfielder.Milner miaka 29 anategemewa kuungana na Wekundu hao July mosi tayari kwa msimu mpya.Milner ameshinda Premier League mara mbil… Read More

0 comments:

Post a Comment