Facebook

Monday, 25 May 2015

BRENDEN RODGERS:WAMILIKI NDIO WENYE MAAMUZI JUU YANGU.

Huku Mashabiki wakipandwa na jazba kwa Timu yao kubamizwa Bao
6-1 na Stoke City hapo Jana, Meneja wao Brendan Rodgers amesema
ataondoka Liverpool ikiwa Wamiliki wake watataka hilo.
Jana huko Britannia Stadium Liverpool waliaaga Msimu wa Ligi Kuu
England kwa kichapo hicho cha Bao 6 na pia kumuaga Kepteni wao
Steven Gerrard ambae anaondoka kwenda kumalizia Soka lake huko
Marekani.
Rodgers amekiri kuwa yuko kwenye presha kubwa baada ya kushinda
Mechi 2 tu katika 9 zilizopita na kumaliza Nafasi ya 6 kwenye Ligi
ikimaanisha Msimu ujao watacheza UEFA EUROPA LIGI.
Pia Rodgers amekiri ni fedheha kwa Timu yao kupigwa Bao 6 kitu
ambacho hakijatokea kwao kwa Miaka 52 na kuwaomba radhi
Mashabiki wao.
Katika Mechi hiyo Brendan Rodgers alimpiga benchi Staa wao
Raheem Sterling ambae amegoma kusaini Mkataba mpya na
kung'ang'ania kuhama.
Hadi Mapumziko Liverpool ilikuwa nyuma kwa Bao 5-0 zilizofungwa
ndani ya Dakika 23 na Mame Biram Diouf, Bao 2, Jonathan Walters,
Charlie Adam na Steven N'Zonzi.
Bao pekee la Liverpool lilifungwa na Steven Gerrard katika Kipindi
cha Pili ambacho pia Stoke walipiga Bao lao la 6 kupitia Peter
Crouch.

Related Posts:

  • HUENDA VIDAL AKATUA ARSENALKLABU ya Arsenal, imeripotiwa kupanga muda wao kwa ajili ya kutangaza usajili wanyota wa Juventus, Arturo Vidal. Vidal alikuwa katika mipango ya usajili ya Manchester United kiangazi mwaka jana lakini walikatishwa tamaa kufua… Read More
  • Falcao arudi rasmi Monaco. Klabu ya Manchester United imedhibitisha kuwa mshambuliaji waliye mchukua kwapo toka timu ya Monaco RADAMEL FALCAO atarudi monaco.Kocha wa Man United Luis Van Gal akiongea alisema "FALCAO ni mchezaji wa hali ya juu na mtu… Read More
  • BRENDEN RODGERS:WAMILIKI NDIO WENYE MAAMUZI JUU YANGU.Huku Mashabiki wakipandwa na jazba kwa Timu yao kubamizwa Bao 6-1 na Stoke City hapo Jana, Meneja wao Brendan Rodgers amesema ataondoka Liverpool ikiwa Wamiliki wake watataka hilo. Jana huko Britannia Stadium Liverpool waliaa… Read More
  • LIVERPOOL KUMTOA SADAKA LAMBERT ILI WAMNASE BENTEKE.KLABU ya Liverpool iko tayari kumtoa Rickie Lambert ili waweze kumsajili Christian Benteke kutoka Aston Villa. Mshambuliaji huyo ni mmoja kati ya nyota waliopo katika mipango ya usajili wa Liverpool majira haya ya kiangazi na… Read More
  • Real Madrid yamtimua Carlo Ancelloti.RASMI: Real Madrid imevunja mkataba na kochawake Carlo Ancelotti baada ya kuinoa kwa miaka miwili.Katika msimu wake wa kwanza Bernabeu, Ancelotti alishinda ligi ya mabingwa, Copa del Rey,  Uefa Super Cup na kombe la klab… Read More

0 comments:

Post a Comment