KLABU ya Arsenal, imeripotiwa kupanga muda wao kwa ajili ya
kutangaza usajili wanyota wa Juventus, Arturo Vidal.
Vidal alikuwa katika mipango ya usajili ya Manchester United
kiangazi mwaka jana lakini walikatishwa tamaa kufuatia Juventus
kutaka kitita cha paundi milioni 40.
Hata hivyo, kutokana na taarifa zilizotolewa hivi karibuni nchini
Italia, Liverpool wameambiwa kuwa wanaweza kumsajili nyota huyo wa
kimataifa wa Chile kwa paundi milioni 25.
Taarifa hizo zinachanganya zaidi baada ya mwandishi wa habari
kutoka Argentina Hernan Feler sasa kudai usajili wa Vidal kwenda
Arsenal umeshakamilika.Mwandishi huyo ambaye anaripotiwa kuwa
ndiye aliyevujisha taarifa za Arsenal kutaka kumsajili Alexis Sanchez
kutoka Barcelona msimu uliopita, aliandika katika ukurasa wake wa
twitter kuwa baada ya michuano ya Copa America klabu itatangaza
rasmi kumsajili nyota huo.
Monday, 25 May 2015
HUENDA VIDAL AKATUA ARSENAL
Related Posts:
Danny Welbeck aelekea Arsenal.Danny Welbeck ameondoka kwenye kambi ya timu ya taifa ya Uingereza inayojiandaa na mechi za kirafiki na anafanyiwa vipimo kwenye klabu ya Arsenal muda huu na anatatajiwa kusaini mkataba kwa mkopo wa muda mrefu - Sky Sports … Read More
Radamel Falcao awasili Carrington tayari kwa vipimo.Hatimaye mshambuliaji Radamel Falcao amewasili uwanja wa Mazoezi wa United,Carrington AON Training Complex tayari kwa vipimo,kusaini mkataba na kisha kutambulishwa kwa waandishi wa habari. Endelea kutembelea www.bantutz.com u… Read More
Dortmund wamekubali dau la Manchester United kwa Mats Hummels.Dortmund wamekubali dau nono la Manchester United juu ya kutaka kumnasa beki kisiki Mats Hummels ~skysport. … Read More
Chicharito atambulishwa Santiago Bernabeu. … Read More
Lewis Holtby ajiunga rasmi Hamburg SV.Kiungo wa Tottenham Lewis Holtby amejiunga na Hamburg ya Ujerumani kwa mkopo hadi mwisho wa msimu. Endelea kutembelea www.bantutz.com. … Read More
0 comments:
Post a Comment