Facebook

Wednesday 27 May 2015

YANGA YAZIDI KUJI IMARISHA,YAONGEZA WENGINE WAWILI.

YANGA SC imeendelea na usajili wa wachezaji wapya kuelekea msimu ujao na leo vifaa viwili vimemwaga wino makao makuu ya klabu,Jangwani.

Beki wa kushoto MwinyiHajji Mngwali amesainimiaka miwili na kipa Benedicto Tinocco kutoka Kagera Sugar amesaini miaka mitatu.

Tinocco nikipa aliyeibuliwa mkoani Mara katika mpango wamaboresho ya timu ya taifa mwaka jana baadaye akasajiliwa Kagera Sugar ya Bukoba, wakati Mngwalini mchezaji wa KMKM ya Zanzibar.

Tinocco yupo timu ya pili ya taifa, Taifa Stars Maboresho wakati Mngwali alikuwepo kwenye kikosi cha Taifa Stars kilichocheza Kombe la COSAFA wiki mbili zilizopita.

Mngwali alicheza mechimoja tu ya mwisho kwenye Kombe la COSAFA mjini Rusternburg, Afrika Kusini Taifa Stars ikilala 1-0 mbele ya Lesotho.

Mechi zote mbili za mwanzo, ambazo Stars ilifungwa 1-0 na Swaziland na 2-0 na Madagascar, beki ya kushoto alicheza Oscar Joshua wa Yanga pia.

Mwinyi sasa anakwendakugombea kucheza bekiya kushoto ya Yanga pamoja na mabeki wengine wawili, Oscar Joshua na Edward Charles ambao wote wapo Taifa Stars.

Tinocco pamoja na kusajiliwa Kagera Sugar msimu huu lakini hakuwa na nafasi kwenye kikosi cha kwanza, ingawa ameonyesha ni kipa mzuri na mwenye umbo zuri, ambaye kama atajibidiisha atakuwa bora baadaye.
Tinocco anakwenda kugombea namba na makipa wazoefu wa Yanga SC, Ally Mustafa ‘Barthez’na Deogratius Munishi ‘Dida’, ambaye kwa sasa ni kipa chaguola kwanza la Taifa Stars.

Wawili hao wanafanya idadi ya wachezaji wapya waliosajiliwa Yanga SC kufika watatu ndani ya siku tatu, baada ya juzi ilimsainisha winga wa Mbeya City, Deus Kaseke kwa miaka miwili.

0 comments:

Post a Comment