Facebook

Monday, 25 May 2015

Said Ndemla amwaga wino Simba SC.

KIUNGO Said Hamisi Ndemla, amesema kwamba ataongeza juhudi ili kukuza kiwango chake na aweze kuisaidia timu yake, Simba SC kushinda mataji msimu ujao.

Akizungumza baada ya kusaini Mkataba mpya wa miaka mitatu na Wekundu wa Msimbazi leo, Ndemla amesema kwamba hiyo ni changamoto mpya kwake.“Kazi yangu nzuri katikamsimu huu imeishawishi klabu kunipa Mkataba mpya.

Hii ni changamoto kwangu, sasa naamini natakiwa kuongeza bidiiya mazoezi ili kukuza kiwango changu na kuisaidia timu yangu,”amesema.

Ameongeza; “Tuna kiu ya mataji, haswa taji la Ligi Kuu (ya Vodacom Tanzania Bara). Dhamira yetu kubwa msimu ujao tufanikishe azma hiyo.

Tunataka ubingwa wa Ligi Kuu,”amesema.Aidha, Ndemla zao la mradi wa soka ya vijana ya SImba SC, amewashukuru viongozi, wachezaji wenzake na benchi la Ufundi kwa ushirikiano wao kwake, ambao umemfanya leoawe mchezaji maarufu.

“Nawashukuru makocha wangu, haswa Matola (Suleiman) ambaye tulikuwa naye tangu Simba B.

lakini nawashukuru viongozi kwa kuniamini, na mimi nawaahidibaada ya kusaini, nitaongeza bidii niisaidie timu,”amesema.

Related Posts:

  • Tambwe afungua akaunti ya magoli.Mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, Khamisi Tambwe ameanza kuonyesha makali baada ya kupiga bao mbili katika mechi ya jana usiku Simba ilipoiadhibu KMKM ya Zanzibar kwa mabao 5-0. Tambwe raia wa Burundi alipiga bao… Read More
  • Wenger apanda ndege kuelekea Roma,Italy Arsene Wenger ameonekana akipanda ndege kutoka London kwenda Rome, Italy. Meneja huyo amekubali kuwa meneja wa timu itakayocheza mechi maalum ya amani, katika mchezo wa soka wa unaojumuisha imani mbalimbali ulioandaliwa na P… Read More
  • Gerrard akabidhiwa jukumu la "kumfunda" Balloteli.Gerrard amepewa jukumu la kumuongoza kimaadili Mario Balotelli kiwanjani na suala la ndani ya klabu litakua juu ya Brendan Rodgers huku Balotelli mwenyewe akiambiwa ajiangalie nje ya klabu kimatendo na kimaadili, kutokufanya … Read More
  • HAYA NDO MAPYA YALIYOBUKA OLD TRAFORD KUHUSU ROJO Mlinzi Marcos Rojo aliyesajiliwa Manchester United kutoka Sporting Lisbon ya Ureno anakabiliwa na shauri la jinai kwao Argentina, na ndilo linamzuia kuanza kuchezea timu yake mpya. Hadi Jumapili hii asubuhi alikuwa hajapatiw… Read More
  • Baada ya "Magumashi" Evodius Mtawala aachia ngazi TFF Mkurugenzi wa wa Vyama na Masuala ya Kisheria katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Evodius Mtawala, amelazimika kuachia ngazi kutokana na sababu mbalimbali. Taarifa ambazo tumezipata, zinaeleza kuwa Mtawala ambaye aliwah… Read More

0 comments:

Post a Comment