Facebook

Saturday, 26 April 2014

Umuhimu wa kula Mboga mbichi za majani huu hapa............



Katika maisha ya binadamu karibu kila jambo zuri linatakiwa kufanywa kwa tahadhari au kuchunga miko yake. Bila ya kufanya hivyo, faida ya jambo hilo haitapatikana na badala yake maafa yatachukua nafasi.

Ulaji wa mboga mboga zikiwa katika hali ya ubichi au zikiwa hazijapikwa una faida kubwa kiafya. Hata hivyo, ulaji huo bila ya kuchukua tahadhari utasababisha magonjwa yanayoenea kutokana na kula vyakula vichafu.


Moto unaharibu


Ni ukweli wa miaka mingi kuwa kupika au kutumia moto katika kuandaa vyakula kuna haribu virutubisho vinavyopatikana katika mboga mboga.


Mboga za majani ambazo hazijakomaa na mbichi ni chanzo kikubwa cha vitamini na madini ya aina mbalimbali. Mboga hizo endapo zitakamuliwa na kutumiwa kama juisi, faida yake kiafya itakuwa kubwa hasa kwa wagonjwa.


Mboga mboga zinaondoa tindikali inayozalishwa wakati vyakula vingine vikisagwa tumboni kama vile nyama na jibini.


Mboga za majani za kijani ni chanzo kikubwa cha carotene ambayo inabadilishwa mwilini na kuwa vitamini A.


Mboga mboga pia, ni chanzo kizuri cha vitamini C.


Vitamini A ina kazi kubwa ya kuimarisha macho ili yaone vizuri hasa wakati wa giza.


Inasaidia pia ukuwaji na ufanyaji kazi wa chembehai na kuimarisha kinga ya mwili.


Vitamini C ina kazi nyingi ikiwemo kuimarisha ufanyaji kazi wa chembehai, inaimarisha kinga, kuponya mafua na vidonda.


Baadhi ya mboga mboga zina protini na wanga. Kwa mfano, maharage na kunde ni chanzo kikubwa cha madini ya chuma na protini. Viazi mviringo na viazi vitamu ni chanzo kikuwa cha wanga.


Wito


Siku hizi kuna kuongezeka kwa tabia ya watu kutumia mboga zikiwa mbichi kutokana na wengi kutambua umuhimu wake.


Tunawahimiza watu watumie mboga mbichi kama vile saladi na kachumbari. Wanaweza kuzitumia zikiwa zimekatwakatwa au kusagwa ili kupata juisi, lakini ni lazima kuzingatia usafi.


Tahadhari


Kwa ushahidi wa kutosha wa kisayansi, ulaji wa vyakula vibichi ambavyo havikuoshwa vizuri ni chanzo kikubwa cha magonjwa ya kuambukiza kama vile homa ya matumbo, kipindupindu, tumbo la kuhara, kuhara damu, kupata minyoo na amweba.


Kwa sababu hiyo, watu wanashauriwa kuosha vizuri mboga mboga kwa kutumia maji safi na salama. Pia, watu wale saladi na wanywe juisi ya mboga mbichi ili kupata virutubisho vingi.


Mboga mboga kama matango, nyanya na karoti, zitumike kutengeneza juisi bila ya kuondoa maganda yake. Kwa sababu maganda yana madini na protini kwa wingi.


Tahadhari nyingine


Watu wawe makini kujua mahali zilipozalishwa mboga mboga wanazizonunua. Miaka michache iliyopita, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kiliwahi kufanya tafiti mbalimbali kuhusu ubora wa mboga mboga zinazozalishwa kando kando ya barabara zinazopita gari na zile zinazozalishwa katika bonde la mto Msimbazi, Jijini Dar es Salaam.


Tafiti hizo zilibaini kuwa baadhi ya mboga zilikuwa hazifai kuliwa na binadamu wala wanyama kutokana na kuwa na kemikali zinazodhuru afya


                                 Imeandaliwa na.....
                                 Katemi methsela(Blogger)
                               0785 442 107

Related Posts:

  • 100's SAMSUNG SECRET CODES   Kwa wale wanaotumia simu za Android basi hizi hapa ni codes ambazo unaweza kuweka na kuona maajabu! * Software version: *#9999# * IMEI number: *#06# * Serial number: *#0001# * Battery status- Memory capacity : … Read More
  • Jifunze hapa "NETWORK SKILLS" Introduction A network is a collection of computers and devices connected to each other. The network allows computers to communicate with each other and share resources and information. History of Netw… Read More
  • IP ADDRESS FULL KNOWLEDGE   An IP address is an identifier for a computer or device on a TCP/IP network. Networks using the TCP/IP protocol route messages based on the IP address of the destination. The Format of an IP Address T… Read More
  • Zitambue simu fake na Original SAMSUNG GALAXY S3 Mambo vipi wadau, naamini tuko salama sote. Leo ningependa kushare nanyi kitu ambacho kimezoeleka sana kuwanacho kwenye mikono yetu lakini kuna kipindi ukikihitaji kile kilicho bora lazima utaikumbuka hii POST.… Read More
  • Use any SIM CARD in any MODEM without unlocking it   Ni shida sana watu wanakuwa nayo kila mtu anataka Ku-unlock Modem yake ili aweze kuitumia laini tofauti na mtandao mmoja husika wa hiyo modem,. Sasa leo wanacomplex tunawekana sawa hapa jinsi ya kutumi… Read More

0 comments:

Post a Comment