Facebook

Thursday, 13 November 2014

Ronaldo akana 'kumponda' Messi

Cristiano Ronaldo amekataa shutma kuwa
amemsema vibaya kinara mwenzie katika
kabumbu, Lionel Messi. kitabu kipya
kuhusu mshambuliaji huyo wa Barcelona,
kinaeleza kuwa mchezaji wa Real Madrid
mara kwa mara amekuwa akitumia maneno
ya kudhalilisha dhidi ya Messi.
Kumekuwa na tetesi kwa muda mrefu juu ya
kutoelewana kwa Ronaldo na Messi.
Ronaldo amesema kuwa hizi ni habari za uongo
na kusema kuwa atachukua hatua za kisheria
kuwashtaki wanaohusika na usambazaji wa
taarifa hizo.
Mchezaji huyo amejitetea kuwa anawaheshimu
wachezaji wenzie wote, akiwemo Messi.
Ronaldo amemaliza ubabe wa Messi wa kutwaa
tuzo ya Fifa ya mchezaji bora wa dunia kwa
miaka mitatu mfululizo, Ballon d'Or baada ya
kutwaa tuzo hiyo mwaka jana.
Zaidi ya yote wanandinga hao wametofautiana
kwa goli moja tu ili kuwa mfungaji bora wa
muda wote kwenye ligi ya mabingwa barani
Ulaya.Messi ana magoli 71 sawasawa na Raul
Gonzales wakati Ronaldo ana magoli 70.
Messi anahitaji magoli mawili tu ili kuwa
mfungaji bora wa muda wote wa ligi kuu ya
Hispania-La Liga,amefunga magoli 250 katika
michezo 285 nyuma ya Telmo Zarra wa
Athletic Bilbao aliyecheza miaka ya
1940-1950.

Related Posts:

  • KARIBU KATIKA MKATE WA PASAKA,NIKIBURUDIKA NA LIGI KUU UINGEREZA.Jana baada ya kuona Majina ya wachezaji katika mechi ya Arsenal na Liverpool niliona vitu viwili kwa haraka haraka, kwanza ni makocha kuwapanga watu wawili wenye bahati nzuri na timu zao msimu huu!!, Kwa Arsenal alikuwepo Oz… Read More
  • COPA ITALIA : JUVE WAINYUKA FIORENTINA 3-0, HAO FAINALI !!Wakicheza Ugenini bila ya Nyota wao bora, Andrea Pirlo , Paul Pogba na Carlos Tevez, Juventus , chini ya Kocha Massimiliano Allegri, Usiku huu wameipindua kipigo cha mechi ya kwanza na kuichapa Fiorentina 3-0 na kutinga Faina… Read More
  • IFAHAMU HISTORIA YA KLABU YA ARSENAL FC.Mwanzo hadi Vita ya Kwanza ya Dunia Maisha ya klabu ya soka ya Arsenal yalianza pale kikundi cha wafanyakazi katika kiwanda cha kuzalisha zana za kivita cha Woolwich walipoamua kuunda klabu ya soka mwishoni mwa mwaka 1886. Kl… Read More
  • IBRAHIMOVIC AFUNGIWA MECHI NNEMshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic amefungiwa kucheza mechi nne za ligi kuu ya Ufaransa baada ya kunaswa na picha za televisheni akitukana. Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Sweden alikasirika na kuwashut… Read More
  • HUU NDIO UZI MPYA WA LIVERPOOL FCRaheem Sterling ambaye wiki iliyopita alikataa mkataba wa kulipwa mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki Liverpool- anaonekana hapa na wachezaji wenzake Martin Skirtel, Simon Mignolet na Daniel Sturridge, wakionesha jezi mpya wat… Read More

0 comments:

Post a Comment