Facebook

Friday, 7 November 2014

WhatsApp yawakaba koo wadanganyifu wote katika mtandao huo.Yaongeza alama za kuonyesha ujumbe uliosomwa na muda uliosomwa.


WhatsApp imewapunguzia sababu za kutojibu wale wote ambao huwa hawajibu ujumbe wa maneno {message} kwa wakatikwa kisingizio kuwa hawakuziona hata kama zilionyesha tiki mbili kuashiria zimefika.Hivi sasa WhatsApp wameamua kufanya mabadiliko katika mtandao huo baada ya kuongeza alama ya kuonyesha kuwa ujumbe umefika na muda uliofika ujumbe huo  kama inavyoonyesha hapa chini
Whatsapp1Kuanzia sasa ujumbe ambao utakuwa umesomwa utakuwa ukionyeshwa kwa tiki mbili za bluu upande wa chini kulia kwenye simu ya mtumiaji na ukibonyeza juu ya ujumbe huo itakuwa ikionyeshwa muda ambao ujumbe huo ulisomwa.

whatsapp2Kabla ya mabadiliko hayo palikuwa na aina mbili tu za tiki,tiki ya kijivu ambayo ilikuwa ikionyesha ujumbe umetumwa na tiki mbili za kijivu zilizokuwa zikiashiria ujumbe umefika.

Kwa upande wa 'Group' tiki mbili za bluu zitakuwa zikionekana pindi tu watu wote kwenye 'group' wakiusoma ujumbe huo 

Ili uweze kuona mabadiliko haya mtumiaji wa WhatsApp unashauriwa ku-Update 'Application' hiyo ya WhatsApp unayoitumia hivi sasa. 

Mabadiliko hayo yamepokelewa tofauti katika mitandao ya kijamii kwa hisia tofauti tofauti, wapo ambao hawajafurahishwa sijui wewe mdau wa Bantu upo katika kundi lipi?

Comment chini utupe mawazo yako katika hili.

Endelea kutembelea www.bantutz.com uweze kuongeza maarifa na kujua mambo mbalimbali.

Related Posts:

  • HIZI NDIZO FAIDA ZA KUNYWA MAJI MWILINI1: Kupunguza uzito: Kunywa maji mengi kunasaidia kupunguza uzito, kwani maji hayana mafuta, kalori wala sukari. 2: Afya ya moyo: Unywaji wa maji mengi kunaweza kupunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo. Utafiti wa miaka … Read More
  • Hii ndiyo simu iliyotengenezwa kwa kutumia nyasi.Watu wengi wamekuwa wakilalamikia teknolojia na ufundi wa simu nyingi za kisasa wengi wakiwaponda wabunifu kwa misingi ya kuwa asilimia kubwa ya simu za mfumo wa 3G na zaidi zinatengezwa kwa plastiki. Sasa basi,bwana mmoja mb… Read More
  • Wanasayansi watengeneza maji yanayozuia risasi.Wanasayansi nchini Poland wametengeza maji ambayo yakipakwa katika vazi linaloweza kukinga risasi ,yanaweza kuzuia risasi mbali na dharubu inayosababishwa na kasi yake kutosababisha madhara ndani ya mwili wa binaadamu. Maji h… Read More
  • Google yapewa wiki 10 kujibu malalamishiHabari kuu ya teknolojia wiki hii ni le ya muungano wa ulaya uliolalamika kwamba Kampuni ya Google ilikuwa ikijipendelea zaidi katika soko lake. Google sasa ina wiki kumi kujibu malalamishi hayo licha ya kusema kuwa haikubali… Read More
  • Hili ndilo jipya kutoka tigo kuhusiana na huduma zao vyuoni. Baada ya wimbi kubwa la wananchi ambao sio wanafunzi kukimbilia sehemu za vyuoni ili kujiunga na huduma nzuri za mitandao hususani dakika za mawasiliano na "internet bundle" leo hii wametangaza zoezi la kuwaandikisha wanafunz… Read More

0 comments:

Post a Comment