Pata kujua kauli mbalimbali za viongozi wa kamati mbalimbali kwenye vikao vya Bunge la Kitiba Mpya vinavyoendelea hivi sasa Mjini Dodoma,viongozi hao wamewasilisha taarifa mbalimbali kutoka kwenye kamati zao,kama utaratibu ulivyopangwa;
Ni maoni ya pande mbili ambazo ni maoni ya wengi ambao ndio wanaounga
mkono serikali mbili alafu maoni ya wachache ambao wanaunga mkono uwepo
wa serikali tatu.
Tundu Lissu: ‘Nusu karne ya
uongo iishe, Tanganyika iliuwawa na amri za Mwalimu Nyerere na hakuwa na
mamlaka kisheria kuiua, hatujawahi kuwa nchi moja, habari ya Tanzania
kuwa nchi moja iliingizwa ktk katiba miaka 20 baada ya muungano, nchi
hii ni haramu…. miaka 50 ya kudanganyana ikome, nchi hii inahitaji
kuelezwa ukweli’
Mchungaji Christopher Mtikila: ‘tulijengwa
kwenye misingi ya uongo ndio maana Mungu alishindwa kubariki hii nchi
yetu kwa miaka 50, uongo tuuondoe, swala la muungano lilikua utapeli wa
kisiasa, tuurudie ukweli kuhusu uhuru wa Watanganyika na Wazanzibari’
Mh Wassira: ‘Hati ya Muungano
ipo, naahidi kwa niaba ya Jamuhuri itawasilishwa kwa Mwenyekiti ndani ya
siku mbili zijazo, kama Wananchi wangetoa maoni kutaka kuvunja
muungano, je tume ingeyaleta? serikali 3 italeta mgongano’
Mh Wassira: ‘Katiba ya Znz ndio
itabakia kuwa sheria kuu kwa Znz kwa mambo yasiyokua ya muungano,
tukiweka serikali 3 hapa zikaweka masharti kuna watu watapata matatizo,
itapunguzia Wazanzibari fursa’
Ismail Jussa: ‘Hoja za historia
kwamba tulikua vipi haziwezi kulibakisha taifa katika mgando, ukiangalia
katiba ya muda ya mwaka 1965 inaendelea kuitambua Tanganyika na kuwepo
makamu wawili wa Rais’
Ismail Jussa: ‘Mkataba wa
muungano haukutoa mamlaka kwa chombo chochote kubadilisha kilichopo
ndani, ajabu bunge limefanya, tunapokua Znz tunasema mengine tukija huku
tunaufyata, Wazanzibari watatuhukumu’
Ismail Jussa: ‘Zanzibar
tumeachwa watupu, tumechoka na hatukubali tena, ktk mfumo wa serikali
mbili Zanzibar haitaweza kujisimamia kamwe, hatutakubali kuendelea nao’
Ismail Jussa: ‘Kama kuna nia njema kwa nini kuna kufichaficha, mfano mwingine hai ni Rais wa Znz kuondolewa kuwa makamu wa Rais’
Unaweza kuchangia mawazo yako hapo chini kama unalolote kuhusu kiako cha leo..............................endelea kupata taarifa na kutembele.............................................
http//www.katemimethsela.blogspot.com
Monday, 14 April 2014
UNAKIJUA WALICHOSEMA TUNDU LISSU, WASSIRA, JUSSA NA MTIKILA KATIKA KIKAO CHA BUNGE LA KITABA MPYA LEO?..Fuatilia Hapa.....
Related Posts:
Ili kunusuru bunge,Sitta aifuta UKAWA Zanzibar.........soma hapa.......... Wakati viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiweka kambi Zanzibar, Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta jana naye alitumia siku nzima visiwani humo akikutana na baadhi ya viongozi wa… Read More
Ingawa Tanzania inapiga vita suala la raia kuwa na uraia wa nchi mbili......Je unawajua vigogo wenye uraia wa nchi mbili soma hapa......!!!!!! katika kufatilia baadhi ya mambo nimepata kufahamu yafuatayo (1)Mh Nyalandu Ana uarai wa Tz na USA (2)Mh Membe Ana urai wa Tz na Canada (3)Mh Letecia Nyerere Ana uraia wa Tz na USA (4)… Read More
Henry Kilewo atupia mtandaoni chat ya Whatsapp ya Ridhiwani na Jerry Slaa wakimponda Lowasa.............fuatilia hapa.................... Kwenye Ukarasa wa Facebook wa Henry Kilewo leo asubuhi nimekutana na hili:"Muoneni huyu anawaza kuwa Rais baada ya kupewa ubunge.... never ever... RZ1 AMSHAMBULIA LOWASSA RZ1 Jakaya Mrisho Kikwete, amemshambulia Edward … Read More
Fahamu kiwango cha elimu kwa kila kiongozi wa Chadema......fuatilia hapa.................... 1) Godbless Jonathan Lema -- Diploma 2) Antony Gervase Mbassa - - Adv diploma - KCMC 3) Prof Kulikoyela Kanalwanda Kahigi --- Phd 4) Freeman Aikaeli Mbowe – Form six 5) Highness Samsoni Kiwia ---- Secondary… Read More
Makala:Historia ya Muungano wa Tanzania...............soma hapa makala hii.... Historia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaanzia April 26 mwaka 1964 siku ambayo Nchi ya Jamuhuri ya Tanganyika ambayo kwa sasa ni Tanzania bara pamoja na iliyokuwa Jamuhuri ya Zanzibar (inayojumuisha Visiwa… Read More
0 comments:
Post a Comment