Pata kujua kauli mbalimbali za viongozi wa kamati mbalimbali kwenye vikao vya Bunge la Kitiba Mpya vinavyoendelea hivi sasa Mjini Dodoma,viongozi hao wamewasilisha taarifa mbalimbali kutoka kwenye kamati zao,kama utaratibu ulivyopangwa;
Ni maoni ya pande mbili ambazo ni maoni ya wengi ambao ndio wanaounga
mkono serikali mbili alafu maoni ya wachache ambao wanaunga mkono uwepo
wa serikali tatu.
Tundu Lissu: ‘Nusu karne ya
uongo iishe, Tanganyika iliuwawa na amri za Mwalimu Nyerere na hakuwa na
mamlaka kisheria kuiua, hatujawahi kuwa nchi moja, habari ya Tanzania
kuwa nchi moja iliingizwa ktk katiba miaka 20 baada ya muungano, nchi
hii ni haramu…. miaka 50 ya kudanganyana ikome, nchi hii inahitaji
kuelezwa ukweli’
Mchungaji Christopher Mtikila: ‘tulijengwa
kwenye misingi ya uongo ndio maana Mungu alishindwa kubariki hii nchi
yetu kwa miaka 50, uongo tuuondoe, swala la muungano lilikua utapeli wa
kisiasa, tuurudie ukweli kuhusu uhuru wa Watanganyika na Wazanzibari’
Mh Wassira: ‘Hati ya Muungano
ipo, naahidi kwa niaba ya Jamuhuri itawasilishwa kwa Mwenyekiti ndani ya
siku mbili zijazo, kama Wananchi wangetoa maoni kutaka kuvunja
muungano, je tume ingeyaleta? serikali 3 italeta mgongano’
Mh Wassira: ‘Katiba ya Znz ndio
itabakia kuwa sheria kuu kwa Znz kwa mambo yasiyokua ya muungano,
tukiweka serikali 3 hapa zikaweka masharti kuna watu watapata matatizo,
itapunguzia Wazanzibari fursa’
Ismail Jussa: ‘Hoja za historia
kwamba tulikua vipi haziwezi kulibakisha taifa katika mgando, ukiangalia
katiba ya muda ya mwaka 1965 inaendelea kuitambua Tanganyika na kuwepo
makamu wawili wa Rais’
Ismail Jussa: ‘Mkataba wa
muungano haukutoa mamlaka kwa chombo chochote kubadilisha kilichopo
ndani, ajabu bunge limefanya, tunapokua Znz tunasema mengine tukija huku
tunaufyata, Wazanzibari watatuhukumu’
Ismail Jussa: ‘Zanzibar
tumeachwa watupu, tumechoka na hatukubali tena, ktk mfumo wa serikali
mbili Zanzibar haitaweza kujisimamia kamwe, hatutakubali kuendelea nao’
Ismail Jussa: ‘Kama kuna nia njema kwa nini kuna kufichaficha, mfano mwingine hai ni Rais wa Znz kuondolewa kuwa makamu wa Rais’
Unaweza kuchangia mawazo yako hapo chini kama unalolote kuhusu kiako cha leo..............................endelea kupata taarifa na kutembele.............................................
http//www.katemimethsela.blogspot.com
Monday, 14 April 2014
UNAKIJUA WALICHOSEMA TUNDU LISSU, WASSIRA, JUSSA NA MTIKILA KATIKA KIKAO CHA BUNGE LA KITABA MPYA LEO?..Fuatilia Hapa.....
Related Posts:
Haiwezekani Bunge kuwa sehemu ya kuficha wezi.. Nimejitokeza kuweka makala hii kimsingi tujadili mambo ya nayoendelea mjengoni, sasa tujadili jambo lililo ibuliwa jana na ndg kafulila,juu ya utafunwaji wa zaidi ya bilioni 200 benki kuu, ni ukweli usiofichika kwa s… Read More
Hajaanza Leo: Warioba ni "Bwana Kero" Tokea Zamani Kama alivyoandikika Edson Kamukana katika makala yake moja "ukiachilia mbali wasomi kadhaa walioamua kulamba matapishi yao na kumtusi Jaji Warioba na wana-CCM wengi wanaotukana bila kujua wanamtusi nani, katikati yake… Read More
Chadema wakiri, wakati umefika wa kuwasamehe Zitto Kabwe na wenzake CHADEMA sasa inapaswa kupitia upya na kufanya masahihisho. kwa maamuzi yote magumu yaliyo wahi kuchukuliwa na vikao vya chama hasa KAMATI KUU.kwakuwa imeweza kutengua msimamo wake na kuvunja serikali kivuli bunge… Read More
Ingekuwa vizuri sana kama huu ushririkiano uliopo wa UKAWA ungekuwa ni wa kudumu..... Bila shaka kila mwananchi anayeitakia mema nchi yetu amevutiwa na habari zilizochapishwa katika gazeti hili jana kwamba vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimeamua kushirikiana katika Ucha… Read More
Mrema aiomba mema ndoa ya CHADEMA,CUF NA NCCR-MAGEUZI MBUNGE wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP ) ametaja ushirikiano wa vyama vitatu vinavyounda kambi rasmi ya upinzani bungeni kwamba ni ndoa ambayo kama wahusika wangekuwa na nia njema, ungeanza siku nyingi tangu Chadema k… Read More
0 comments:
Post a Comment