Facebook

Friday, 16 May 2014

Aliyefichua kanda ya Jay-Z akishambuliwa afutwa kazi


Solange alimshambulia Jay Z katika lift walipokuwa wanatoka tamashani
Mfanyakazi aliyefichua kanda inayoonyesha mwanamuziki Jay Z akishambuliwa na shemeji yake , amefutwa kazi.
Kamera ya lifti ilinasa vurumai kati ya Jay Z na shemeji yake Solange Knowles aliyeonekana kuwa na hasira mno huku akimshambulia Jay Z , ingawa haijulikani kilichosababisha vita hivyo kwenye lifti.
Kanda hiyo ya video ambayo ilitolewa kwanza kwenye tovuti ya udaku kuhusu watu maarufu TMZ, ilimwonyesha dadake Beyonce akimpiga Jay Z baada ya tamsha la Met mjini Los Angeles, iliyofanyika mwezi Mei tarehe 5.
Baada ya ugomvi mkali baina yao, mlinzi aliingilia kati. Hata hivyo kanda hiyo haikuwa na sauti.
Hoteli hiyo inayojulikana kama ‘The Standard ilisema kuwa ilishtushwa sana na kufichuliwa kwa matukio ya Lifti na ikamtaja mfanyakazi huyo aliyehusika katika ufichuzi huo.
Mfanyikazi huyo alifutwa kazi kwa kosa la kuvunja sheria za usalama kwa kufichua video za CCTV, ambazo ni za siri.
Hoteli hiyo iliongeza kuwa ingetoa habari zingine zote za ziada kwa idara ya kupambana na wakiukaji wa sheria.
Waakilishi wa Jay Z, Beyonce na Solange hawajasema lolote kuhusiana na tukio hilo.

Related Posts:

  • Mwanamziki apasuliwa huku akiimba. Alama Kante afanyiwa upasuaji Katika tukio la kwanza la aina yake mwanamziki mmoja nchini Ufarasa amefanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe kooni huku akiimba. Madaktari wanasema hatua hiyo ilichukuliwa ili kuepuka kuharibu… Read More
  • Unamjua kidume anayemfaidi Agnes Masogange ? Kama mnavyojua dada yetu Masogange kwa muda sasa yupo nchini South Africa na amekuwa sio mchoyo wa picha zake, wakati wote amekuwa anashare nasi picha zake kupitia ukurasa wake wa Instagram Sasa mimi sijajua Sauzi… Read More
  • Lulu tena !  Si mwingine ni yule yule Elizabeth Michael A.k.A LuLu.....Hii ni moja ya picha zake zilizosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Normal 0 false false false EN-US X-NO… Read More
  • Wema akana kuwa na Mimba ya Diamond !   Staa wa movie Tanzania a.k.a Mrs. Diamond Platnumz ameamua kuandika ukweli kuhusu stori ulizosikia kwamba kwa sasa ni mjamzito… Kupitia page yake ya instagram Wema ameandika ‘Jamani hizi habari za mimi kuwa pregn… Read More
  • Gwiji Michael Schumacher atoka kwenye 'coma' Michael Schumacher alikuwa akitibiwa kwenye hospitali ya Chuo Kikuu cha Grenoble nchini Ufaransa. Bingwa wa Formula 1 Michael Schumacher ameondoka hospitali mjini Grenoble na hayupo tena kwenye coma, imeeleza f… Read More

0 comments:

Post a Comment