Facebook

Thursday 29 May 2014

Van Gaal awakataa Kroos na Fabregas, anawataka Strootman na makinda wa Feyenoord

LOUIS_VAN_GAAL
ZIMEZAGAA ripoti huko Ulaya kwamba Meneja mpya wa Manchester United Louis van Gaal hana nia ya Toni Kroos wa Bayern Munich na Cesc Fabregas na badala yake anawataka Wachezaji wa Uholanzi ambayo ndie Kocha wa Timu ya Taifa.MARTIN_INDIS
Akiwa Kambini pamoja na Timu ya Holland inayojitayarisha kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza huko Brazil hapo Juni 12, imedaiwa Louis van Gaal anataka kuwachukua Wachezaji wawili walioko Kambini humo wanaochezea Klabu ya Feyenoord, Jordy Clasie and Bruno Martins Indi, ili wajiunge nae Old Trafford mara baada ya Kombe la Dunia.
Pamoja na hao, pia inasemekana LVG anamtaka Mchezaji wa AS Roma, Kevin Strootman, licha ya kuwa sasa yupo muda mrefu nje ya Uwanja akiuguza Goti lake badala ya Kiungo waJordy_Clasie Barcelona, Cesc Fabregas.
Watatu hao, Clasie, Indi na Strootman, ni Waholanzi wenye sifa kemkem za umahiri mkubwa kiasi ambacho LVG sasa ameuagiza Uongozi wa Man United uanze mazungumzo Klabu zao na kumaliza kazi ya Uhamisho wao kimya kimya ili isije ikaonekana kama yeye, ambae ni Kocha wa Uholanzi, ametia mkono wake.
Indi na Clasie, wote wakiwa na Miaka 22 kila mmoja, wamejipatia sifa kubwa Klabuni kwao Feyenoord kiasi ambacho Clasie Msimu huu amelazimika kuchukuliwa Timu ya Taifa ya Holland na pia Nahodha wa Holland, Robin van Persie, ambae pia ni Mchezaji wa Man United, kukiri Clasie ni Paul Scholes mpya.
Nae Bruno Martins Indi, Sentahafu Mrefu, mwenye nguvu na akili, ni nguzo imara ya Feyenoord na Holland.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata taarifa mbalimbali za usajili

0 comments:

Post a Comment