Facebook

Friday 30 May 2014

Pep Guardiola amuoa mchumba wake waliyezaa nae watoto 3

2,w=650,c=0.bildHatimaye kocha wa klabu bingwa ya Ujerumani Bayern Munich, Pep Guardiola amefunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Cristina Serra leo hii, na bosi huyo wa Bayern na mchumba wake waaliamua kufanya ndoa hiyo kwa kawaida kabisa bila shamra shamra zozote.
Ndoa hiyo imefungwa kiserikali huko Matadepera, Catalonia, Spain.
Pep na mchumba wake Cristina, kwa pamoja na watoto wao watatu na wazazi wao, walifanya sherehe ndogo kuhalalisha mapenzi yao.
Tazama picha hapo chini namna ndoa ya Guardiola ilivyokuwa
o_MDSIMA20140529_0125_1
Guardiola mwenye shati la kaki na mkewe Cristina mwenye suruali nyeusi pamoja kti jekundu wakisindikizwa na ndugu zao kwenda kufunga ndoa.
i_MDSIMA20140529_0126_1

0 comments:

Post a Comment