Facebook

Thursday, 29 May 2014

Kumeibuka Mabishano makubwa kati ya Papa na Kiongozi wa Israel,Netanyahu kuhusu lugha ya Yesu...fuatilia hapa..

      Yerusalemu, Israel. Malumbano makali ya maneno na hoja yamezuka baina ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kuhusu lugha gani aliyotumia Yesu Krtisto miaka 2,000 iliyopita.
Viongozi hao Jumatatu mchana wakati wa ziara ya siku tatu ya Papa aliyoifanya katika eneo la Mashariki ya Kati ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu atwae wadhifa huo. “Yesu aliishi hapa katika ardhi ya nchi hii. Alizungumzia Kiebrania,” alianza Netanyahu wakati akimweleza Papa Francis kwenye mkutano wa hadhara mjini Yerusalemu.
Netanyahu, pia akaeleza kuwa upo uhusiano wa karibu baina ya mahali alikozaliwa Yesu na Ukristo.
Naye Papa Francis akasikiliza kwa muda, kisha akajibu: “Yesu alizungumza lugha ya Kiaramaiki.”
“Ndiyo, nimesema alizungumza Kiaramaiki, lakini pia alijua Kiebrania,” akaingilia kati Netanyahu.
Hata hivyo, mjadala huo umepokewa kwa hisia tofauti na watu wengi ambao wamekuwa wakifuatilia ziara ya siku tatu ya Papa Francis katika nchi takatifu.
Mtaalamu wa masuala ya lugha, raia wa Israel, Profesa Ghil’ad Zuckermann ameliambia Shirika la Habari la Reuters kwamba wawili hao, Netanyahu, ambaye ni mtoto wa mtaalamu wa historia ya Kiyahudi na Papa Francis, kiongozi wa kiroho anayeongoza waumini bilioni 1.2 Wakatoliki, kila mmoja ana hoja. “Yesu alikuwa mzungumzaji wa Kiaramaiki,” anasema Profesa Zuckerman kuhusu lugha hiyo ambayo imetoweka yenye uhusiano na Kiebrania. “Pia, anaweza kuwa alizungumza na kufahamu Kiebrania, lugha ambayo ilitumika kwenye maandiko.”
Prof Zuckermann alisema kuwa wakati wa Yesu, Kiebrania kilizungumzwa na watu wa madaraja ya chini - “ambao ndiyo aliowahubiria”. Mojawapo ya vitu vingi katika eneo la Mashariki ya Kati hadi sasa ni kuhusu utata wa Yesu, utata huo umechukua pia sura na mtazamo wa kisiasa.
Yesu, Myahudi alizaliwa kwenye mji wa Bethlehemu ambao ulikuwa chini ya himaya ya Warumi, kwenye Mkoa wa Yudea, katika ardhi inayoshikiliwa kwa sasa na Israel kwenye Ukanda wa Magharibi.
Alikulia mjini Nazareth , akaendesha utume kwenye mji mwingine wa Galilea, ambao pia uko kaskazini mwa Israel, alifia mjini Yerusalemu, mji ambao unatukuzwa na Wayahudi, Wakristo na Waislamu, ambao unagombewa na tawala za Israel na Palestina hadi sasa.
Kwa upande wao, Wapalestina wamekuwa wakidai kuwa Yesu ni Mpalestina. Hata hivyo, utawala wa Israel umekuwa ukipingana na mtazamo huo.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua visa na visanga tofauti tofauti vinavyotokea duniani.

Related Posts:

  • Apple wazindua bidhaa mpya.Kampuni ya Apple imezindua saa ya kisasa - the Apple Watch - ambayo ni bidhaa yake mpya tangu iPad ya kwanza na tangu kifo cha mmoja wa waasisi wake Steve Jobs. Kifaa hicho huendesha programu tumishi (apps) na pia hufuatilia … Read More
  • Mtanzania ateuliwa kuwa makamu mkuu wa Rais wa BET Networks.  BET Networks, ambayo ipo chini ya kampuni ya Viacom Inc. imetangaza kumwajiri Kay Madati kama makamu mkuu wa rais (Executive Vice President) na pia kama Chief Digital Officer. Madati, raia wa Tanzania aliyeishi katik… Read More
  • Nyangumi apatikana Mtwara.Mzoga wa samaki aina ya nyangumi Umepatikana katika pwani ya Bahari ya Hindi Mkoani Mtwara na kisha kuvutwa Kuelekea majini na wavuvi wa Kata ya Msangamkuu. Mzoga huo una urefu wa futi 48 na uzito unaokadiriwa kuwa zaidi ya t… Read More
  • Wanafunzi 12,000 wakosa nafasi Vyuo vikuu,TCU yawapa nafasi ya Pili.Wanafunzi 12, 000 wakosa nafasi za vyuo vikuu, TCU yawapa nafasi ya pili kuchagua nafasi za masomo (course) ambazo bado ziko wazi na wameshauriwa kutochagua "course" zenye ushindani mwingi maana hii itasababisha wengine kukos… Read More
  • MIFUPA YA DINOSARIA "GODZILLA" YAPATIKANA TANZANIAAina mpya ya dinosaria imetambuliwa kufuatia kupatikana kwa mifupa nchini Tanzania. Mabaki hayo ya dinosaria yaliyopewa jina la - Rukwatitan Bisepultus - yalipatikana katika korongo moja kwenye eneo la Rukwa, kusini magharibi… Read More

0 comments:

Post a Comment