Facebook

Saturday, 31 May 2014

Matamshi kuhusu ubakaji yakera India


Matamshi ya mwanasiasa mmoja mwanamke nchini India kuhusu ubakaji yamelaaniwa na watu wengi kote nchini humo.
Asha Mirge, ambaye ni mwanachama wa kikundi cha viongozi wanawake serikalini katika jimbo la Maharastra, amesema kuwa wanawake pia wanachangia pakubwa kwa wao wenyewe kubakwa kutokana na mavazi pamoja na wanavyotembea na hata kuzungumza.
Amehoji kwa nini wanawake hutoka nje nyakati za usiku.
Matamshi haya yaliyozua gumzo katika vyombo vya habari kote nchini India, yamesababisha kero kubwa kutoka kwa makundi ya wanaharakati wa maswala ya wanawake na wanasiasa wengine.
Bi Mirge hata hivyo ameomba radhi kwa matamshi yake akisema yametiwa chumvi.
Inda imekuwa ikimbwa na visa vya mara kwa mara vya ubakaji kiasi cha serikali kubuni sharia kali dhidi ya wabakaji.
Ni wiki jana tu ambapo wazee wa kijiji waliamrisha kubakwa kwa mwanamke ambaye alikuwa na uhusianao wa kimapenzi na mwanamume ambaye sio wa kutoka jamii moja naye.

Related Posts:

  • Kumbe mhadhiri UDSM ndio Rais mpya wa Malawi Kwa ushindi wa Profesa Mutharika katika kiti cha urais wa Malawi, anaongeza idadi ya jamii ya wasomi waliopitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ama wakiwa wahadhiri au wanafunzi, kwani alifundisha chuoni … Read More
  • Mutharika rais mpya nchini Malawi   Mgombea wa Chama cha upinzani nchini Malawi Peter Mutharika ametangazwa mshindi katika uchaguzi wa urais uliozua utata. Mutharika wa Chama cha Democratic Progressive Party amepata asilimia 36.4 ya kura, imetangaz… Read More
  • Meli yalipuka Bandarini huko Japan...    Mlipuko mkubwa umetokea kwenye meli kubwa ya mafuta nchini Japan katika Pwani ya Kusini Magharibi mwa bandari ya Himeji na kusababisha mtu mmoja kati ya wanane waliokuwa ndani ya meli hiyo kupotea huku wengi… Read More
  • China yakusanya hawa watu Uwanja wa Mpira na kuwahukumu kifo.   Watu 55 nchini China wamekumiwa kutumikia adhabu mbalimbali kwa makosa ya ugaidi, uhalifu wa kutumia silaha pamoja na mauaji, hukumu iliyotolewa katika Jimbo la Kaskazini Magharibi la Xinjiang mbele ya umati m… Read More
  • Matamshi kuhusu ubakaji yakera India Matamshi ya mwanasiasa mmoja mwanamke nchini India kuhusu ubakaji yamelaaniwa na watu wengi kote nchini humo. Asha Mirge, ambaye ni mwanachama wa kikundi… Read More

0 comments:

Post a Comment