Facebook

Friday 30 May 2014

Anti Lulu na bwana ake mpya wapigana chini

LILE penzi la msanii wa filamu na mtangazaji, Lulu Mathias na mchezaji mpira wa zamani, Amani limesambaratika baada ya hivi karibuni mwanaume huyo kuondoka na kilicho chake huku akimwacha mwanadada huyo ndani ya nyumba peke yake.

Chanzo chetu makini kilisema kuwa, tukio hilo lilitokea hivi karibuni huko Majohe walipokuwa wakiishi wawili hao ambapo mwanaume huyo aliamua kuondoka na kurudi nyumbani kwao na kumuacha Aunty Lulu ndani ya nyumba hiyo waliyokuwa wamepanga.


Baada ya kuzipata habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Aunty Lulu, akafunguka:

“Ukweli mimi na Amani tumeachana kwani kipigo kimenizidi kila kukicha isitoshe ndugu zake hawanipendi, nimebaki peke yangu kwenye nyumba tuliyokuwa tumepanga huku Majohe na yeye ameondoka na vitu vyake vyote, amerudi kwao.”


Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata habari mbalimbali kwa wakati na muda muafaka.











0 comments:

Post a Comment