Facebook

Wednesday 28 May 2014

Ulinzi waimarishwa kombe la dunia Brazil.....Unajua ni wanajeshi na polisi wangapi wamepangwa !!!!

 brazuka

Mawaziri wa ulinzi nchini Brazil wameweka wazi kuwa zaidi ya vikosi vya kijeshi laki moja na nusu (150,000) vitasambazwa nchini humo kuhakikisha kunakuwa na usalama wa kutosha wakati mashindano ya mwaka huu ya kombe la dunia.
Kwa mara ya kwanza mpira unarejea katika ardhi yake ya nyumbani kwa zaidi ya miaka 60 wakati Brazil ikiwa katika maandalizi ya mwisho ya kuwa mwenyeji wa michuano hiyo mikubwa zaidi duniani ambapo kwa kiasi fulani hali ya usalama imeonekana kuwa si nzuri kufuatia maandamano ya hapa na pale.
brazuka2
Kumekuwa na maandamano ya wananchi wenye hasira wasiotaka mashindano hayo yafanyike, wengi wamekuwa na hasira juu ya kiasi cha pesa kilichotumika kwa ajili ya maandalizi yake zaidi katika kipindi ambacho nchi inakabiliwa na mtikisiko wa kiuchumi.

0 comments:

Post a Comment