Facebook

Friday 30 May 2014

Brad Pitt ashambuliwa huko Los Angeles

Vitalii Sediuk aliondolewa katika sehemu hiyo na polisi waliomfunga pingu
Mwanamume mmoja amekamatwa baada ya kumshambulia kwa makonde muigizaji maarufu duniani Brad Pitt usoni mwake katika sherehe ya ufunguzi wa filamu ya Maleficent mjini Los Angeles.
Mwandishi habari wa Ukraine Vitalii Sediuk - anayejulikana kwa kuwahahadaa watu mashuhuri duniani ,aliripotiwa kuonekana akivuka kizuizi na kumkumbatia Brad kabla ya kumpiga usoni.
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 25 kwa jina Vitalii Sediuk, alikamatwa na walinzi wa Brad baada ya kupambana naye na kukabidhiwa kwa polisi waliokuwa wanshika doria.
Sediuk aliondolewa na polisi katika tamasha la filamu la Canes wiki jana baada ya kuingia bila idhini
Pitt alikuwa anakutana na mashabiki wake kabla ya kushambuliwa ingawa hakujeruhiwa vibaya.
Inaaminika kuwa Pitt alipigwa usoni ingawa polisi wanachunguza kisa hicho
Pitt na mkewe Angelina Joli ndio waigizaji nyota katika filamu hiyo mpya ya Maleficent ambayo ilikuwa inazinduliwa na kampuni ya Disney.
Msemaji wa kampuni ya Disney iliyotengeza filamu hiyo alisema kuwa walisikitishwa na kitendo hicho na kwamba polisi wanafanya uchunguzi.
Sediuk alizuiliwa na polisi Jumatano usiku akisubiri kuachiliwa kwa dhamana ya dola 20,000.
Polisi walisema kitendo cha kijana huyo kilikuwa cha maksudi ingawa uchunguzi bado utafanywa.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata stor mbalimbali zinazowahusu mastaa mbalimbali kutoka katika kila kona ya dunia.Jukumu letu sisi ni kukuhabarisha.

0 comments:

Post a Comment