Facebook

Saturday 31 May 2014

Beyonce atupia picha akiwa analea mtoto nyumbani kwake

 
 Msanii maarufu wa Marekani Beyoncé ame 'share' picha za familia yake kwenye tovuti yake kuonesha upande wake kama 'mama' kutokana na wengi kuzoea kumuona kama muimbaji akishambulia jukwaa.
Katika picha hizi anaonekana akimbembeleza mwanaye Blue Ivy alale. Picha nyingine mwanaye huyo anaonekana akijaribu kuvaa viatu vya mama yake. Nyingine inaonesha baba wa Blue Ivy (ambaye ni Jay Z kama hujashtukia) akipiga misele kwa pikipiki. Nyingine anaonesha style yake ya rasta na mapozi ya kimtindo.
Bila shaka anatuonesha kuwa licha ya kuwa bize na kufyatua album na 'singo' nyingi, za 'kutisha' bado ana muda wa kulea na kuwa kama 'mama wa kawaida'. Hii unaweza ku- share na masharo.

 
 
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata stori mbalimbali zinazowahusu wasanii mbalimbali.

0 comments:

Post a Comment