Tuesday, 6 May 2014
Uchunguzi kumbe Makalio Makubwa Kuna Vingi Ndani Yake
Uchunguzi uliofanywa nchini Uingereza umeendelea kulipandisha chati umbo la kibantu, kwa kusema kwamba, kuwa na unene zaidi eneo la mapajani, katika makalio na katika mahips ni vizuri kiafya, na humzuia mtu asipate matatizo ya kiafya.
Wataalamu wanasema kuwa, mafuta yanayopatikana katika mahips, huondoa fati asidi mbaya kiafya ambazo huwa na mada za kuzuia uvimbe ambazo huifanya mishipa ya damu isizibe. Timu hiyo ya wachunguzi imesema kuwa, makalio makubwa ni bora kuliko mafuta ya zaida yanayojilundika katika mzunguko wa kiuno, ambayo hayasaidii chochote.
Wachunguzi hao wamesema katika Jarida la Kimataifa la Obesiti kwamba, sayansi inapaswa kuangalia jinsi ya kuongeza mafuta katika eneo la mahips na pengine katika siku zijazo madaktari watatakiwa kuangalia njia za kuyahamisha mafuta mwilini na kuyapalekea katika sehemu za mahips ili kulinda afya za watu kutokana na magonjwa ya mishipa ya moyo na magonjwa mengineyo kama kisukari.
Watafiti hao wameeleza kwamba, kuwa na mafuta kidogo katika hips kunaweza kupelekea matatizo makubwa ya umetaboli.
Wataalamu hao wameendelea kusema kwamba, ushahidi unaonyesha kwamba, mafuta yanayozunguka mapaja na sehemu za nyuma ni vigumu kuyeyuka kuliko yale yaliyo katika kiuno.
Ingawa suala hilo linaonekama kana kama ni kinyume, lakini ni kweli kwamba kutoyeyuka huko kuna faida kwani, wakati mafuta yanapoyeyuka kwa urahisi hutoa mada inayoitwa cytokines ambayo huleta uvimbe katika mwili.Mada za cytokines zinahusiana moja kwa moja na magonjwa ya moyo na kisukari. Kuyeyuka taratibu kwa mafuta katika mapaja pia husababisha homoni ya adiponectin izalishwe kwa wingi na husaidia kudhibiti sukari katika damu na jinsi mafuta yanavyochomeka.
Dakta Konstantinos Manolopoulos aliyeongoza utafiti huo kutoka chuo kikuu cha Oxford amesema kuwa, la muhimu ni umbo na wapi mafuta yanakusanyika, na kwamba unene wa mahips na mapaja ni mzuri kuliko unene wa tumbo.
Related Posts:
Orodha ya ya watu 10 wenye IQ kubwa duniani … Read More
Vijana 3 wamekamatwa wakitaka kuiba sanamu ya Bikira Maria kanisani.Na hiki ndicho kilichowakuta Vijana watatu Songea wametakiwa kwenda na wazazi wao kutubu dhambi za kutaka kuiba sanamu la Bikira Maria katika Kanisa Katoliki la Kigango cha Samora. Katekista wa Kigango hicho Keneth Mhagama walisema vijana ha… Read More
Yule gwiji katika uandishi wa vitabu na mtaalamu wa fasihi,Ngugi wa Thiong'o atunukiwa shahada ya udaktari Ujerumani Ngugi wa Thiong’o ametunukiwa shahada ya Udaktari wa heshima na Chuo Kikuu cha Bayreuth cha Ujerumani, huku vitabu vyake “Shetani Msalabani” na “Matigari” vikiwa vimempatia umashuhuri na mashaka pia nchini mwake… Read More
Hilo ndilo gari linaloweza kujiegesha kwa kutumia saa. Hakuna kitu kibaya kama kusahau ulikoegesha gari lako katika jengo la kuegeshea magari lenye gorafa nyingi. Lakini hivi karibuni hautahihajika kupanda gorofa kutafuta gari lako kwani kampuni ya kutengeza magari ya BMW, i… Read More
Bill Gates anywa maji yaliyotokana na kinyesi cha binaadamu Mmiliki wa kampuni ya Microsoft, Bill Gates anywa maji yaliyotokana na kinyesi cha binaadam kuonyesha teknolojia itakayosaidia maji safi katika nchi zinazoendelea. Bill Gates amesema maji "yana ladha nzuri tu … Read More
0 comments:
Post a Comment