Facebook

Thursday 15 May 2014

Alichosema Rio Ferdinand kuhusu Kuondoka Man Utd na Hatma Yake,,,,,,


Jana usiku maisha ya kisoka ya beki wa kimataifa wa England Rio Ferdinand ndani ya klabu ya Manchester United yalifikia mwisho baada ya kutangaza kwamba ameamua kuachana na klabu hiyo.
Rio Ferdinand ambaye alijiunga na Manchester United mnamo mwaka 2002 kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya uhamisho paundi millioni 29.5 ameshaitumikia United kwenye michezo 454 na amemaliza mkataba wake na klabu hiyo na pande zote mbili zikaamua kutoongeza mkataba mpya.
Muda mfupi baada ya taarifa kuzagaa kwenye mitandao kuhusu kuondoka United, Ferdinand alitumia mtandao wake binafsi kutoa rasmi taarifa ya kuondoka Old Trafford.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com ili uweze kupata taarifa mbalimbali zinazohusiana na usajili barani ulaya na Afrika kwa Ujumla

0 comments:

Post a Comment