Giggs awaasa mashabiki wa Man United Ufanisi utarejea
Kaimu kocha wa Manchester United
Ryan Giggs amewarai mashabiki wa klabu hiyo maarufu kuwa wasife moyo
ushindi utarejea Old Trafford katika siku za usoni.
Kigogo huyo wa Manchester United aliwaasa
mashabiki punde baada ya kuingoza Manchester united kuilaza Hull city
mabao 3-1 katika mechi yao ya mwisho ya nyumbani msimu huu wa ligi kuu
ya premia ya Uingereza.Kaimu kocha huyo mwnye umri wa miaka 40 alifunga ukurasa wa kipindi chake huko Old Trafford kwa kumkaribisha uwanjani kizazi kijacho cha wachezaji wa timu hiyo alipomkaribisha chipukizi James Wilson.
Tineja huyo alifunga mabao mawili kabla ya Robin van Persie kutamatisha kichapo hicho.
Mashabiki wamuomba Giggs asiondoke Man United
"Kwa muda mrefu tumeshuhudia msururu wa matokeo ya kuridhisha hapa Man united kwa hivyo hiki kipindi cha matokeo duni hautadumu kwa muda mrefu itapita. Na sote tutafurahia tena umaaruufu wa Manchester United tunayoijua"
Ryan Giggs
Mechi hiyo itakuwa siku ya Jumapili.
Hadi kufikia sasa, kocha Louis van Gaal ndiye anayepigiwa upatu kuchuakua hatamu kama mkuu wa kiufundi Old Trafford ijapokuwa tangazo rasmi linasubiriwa wakati wowote kabla ya mechi dhidi ya Southampton.
0 comments:
Post a Comment