Facebook

Thursday, 8 May 2014

Mamia wauawa na Boko Haram Nigeria.............




Juhudi za serikali dhidi ya kundi hilo hazijaonekana kuzaa matunda
Taarifa kutoka nchini Nigeria, zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa katika shambulizi lililofanywa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram katika mpaka wa nchi hiyo na Cameroon siku ya Jumanne.
 Kiongozi mmoja wa eneo hilo, Ahmed Zanna, alisema kuwa washukiwa walivamia mji wa Gamboru Ngala, katika jimbo la Borno, na kuwaua takriban watu 300.
Inaarifiwa wapiganaji hao waliwafyatulia risasi watu kiholela katika soko kuu la eneo hilo.
Wandishi wanasema nchini Nigeria  ilikuwa vigumu kupata taarifa hizo mapema kwa sababu ya changamoto ya mawasiliano katika jimbo hilo hasa kwa sababu eneo hilo liko mbali sana.
Wakazi wa eneo hilo wanasema kuwa walipata zaidi ya maiti miamoja kutokana na shambulizi hilo.

Related Posts:

  • Rais mpya wa Malawi aingia rasmi madarakani leo Rais Mutharika akikagua gwaride katika uwanja wa Kamuzu Maelfu ya watu wamehudhuria sherehe za kukabidhiwa mamlaka kwa Rais mpya Peter Mutharika. Bwana Mu… Read More
  • Marekani ilikosea kuwaachilia Taliban 5 wazazi wa Bowe Serikali ya Afghanistan imeghadhabishwa na makubaliano ya Marekani kukubali kuwaachia huru wanamgambo watano wakuu wa Taliban, ili kuachiwa huru kwa mwanajeshi wa Marekani. Wafungwa hao kutoka g… Read More
  • Wanawake wabakwa gerezani - DRC Wanawake wabakwa gerezani DRC Utafiti uliofanywa na shirika moja la misaada Uingereza umeonyesha kuwa ubakaji unatumiwa tena kwa kiasi kikubwa gerezani kama adhabu kwa wanawake wanaojihusisha na masuala ya siasa … Read More
  • Mlipuko mwingine Nigeria - 14 wauawa Nigeria yashambuliwa Polisi Kaskazini mashariki mwa Nigeria wanasema kuwa shambulizi la bomu limewauwa zaidi ya watu 14 na kuwajeru… Read More
  • Mfalme wa Uhispania aachia ngazi Familia ya Carlos imekumbwa na kashfa za ufusadi na uwindaji haramu Mfalme wa Uhispania Juan Carlos anaachia mamlaka, waziri mkuu Mariano Rajoy ametangaza. Juan Carlos, mwenye umri wa miaka 76, amekuwa mfalme tangu … Read More

0 comments:

Post a Comment