Tuesday, 6 May 2014
Kinana Amtaka Maalim Seif Ajiuzulu
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Sharif Hamad, kama kweli hataki Muungano wa serikali mbili, amuandikie barua Rais wa Zanzibar, Dk Mohamed Shein na kujiuzulu wadhifa wake wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Tamko hilo lilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara, uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.
Kinana alisema anachokifanya Seif ni sawa na kuwaramba vichogo wanasiasa wenzake wa upinzani, wakati yeye akipata mshahara na marupurupu mengine, yanayomwendeshea maisha yake chini ya serikali ya CCM.
Alisema kama kweli Maalim Seif anajigamba ni jasiri, achukue uamuzi sahihi wa kujiuzulu wadhifa wake, ili apate nafasi ya kutosha kuwatumikia wananchi nje ya Serikali.
Kinana alieleza kuwa kutembea nchi nzima kwa Seif, si kitendo cha uungwana kufanywa na kiongozi mwenye wadhifa wa Makamu wa Kwanza wa Rais, akiwa ndani ya Serikali inayomlipa mshahara na huduma nyingine muhimu, akaamua kuwachochea wenzake, ambao wako nje ya Serikali kuleta chokochoko dhidi ya Serikali anayoitumikia.
Maalim Seif ameshatuhumiwa kuwa kigeugeu katika maisha yake ya kisiasa, ambapo hivi karibuni Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Mohammed Seif Khatib, alielezea namna kiongozi huyo wa CUF, alivyowahi kuwa mtetezi wa serikali mbili alipokuwa kiongozi katika Serikali ya CCM, ambako alitumia nguvu kubwa kupinga vuguvugu la kudai serikali tatu mwaka 1984.
Related Posts:
Angalia katika Picha Namna Wajumbe wa Bunge La Katiba Kutoka Upinzani Walivyogoma Na kutoka Nje Ya ukumbi wa Bunge Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba ambao wanaunga mkono mfumo wa Serikali za tatu wakitoa katika Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma baada ya kususia kikao Wajumbe wa Bung… Read More
Sababu za Upinzani Jana kususia kikao cha bunge hizi hapa...... Leo katika kipindi cha Kumepambaz kinachorushwa hewani na kituo cha Radio cha RADIO ONE STERIO alisikia Kamanda Aikael Freeman Mbowe akitoa ufafanuzi wa UKAWA kutoka nje ya bunge maalumu la katiba na kutorudi tena b… Read More
Mwiguli "asiyefanya kazi na asile".. Ukawa Kunyimwa Posho Bungeni.....fuatilia hapa.......... Ni Siku ya pili tangu Wajumbe wa Bunge la Katiba Kutoka Vyama vya Upinzanii wanaounda kitu kinachoitwa UKAWA wasusie Shughuli za Bunge la Katiba kwa Madai wamechoka Kutukana na Kuburuzwa kwenye Bunge hilo. Hii leo Naibu… Read More
Rais Kikwete akerwa na Wanasiasa kumtukana Mwalimu J.K.Nyerere...soma hapa barua aliyoiandika.......... Rais Kikwete akerwa na kitendo cha wanasiasa kumtukana muasisi wa Taifa hili Mwalimu Nyerere....Asema ni utovu wa nidhamu kuwatukana waasisi wa Tanzania hususan Mwalimu J.K Nyerere na Sheikh Abeid Aman Ku… Read More
Upinzani Watoa Tamko lao leo kuhusu kugomea Vikao Vya Bunge....soma soma kauli zao mbalimbali hapa...... Baada ya kugoma na kuamua kutoka nje ya bunge la katiba Dodoma kikundi cha umoja wa katiba ya Wananchi (UKAWA) kimekutana na waandishi wa habari April 17 2014 na kuyazungumza haya yanayofata hapa chini… Read More
0 comments:
Post a Comment