Tuesday, 6 May 2014
Mrisho Ngasa" Azam Wametushika Pabaya"
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Mrisho Ngassa amesikia taarifa za kuondoka kwa Didier Kavumbagu na Frank Domayo akatamka: “Aisee hilo ni pigo kubwa kwa kikosi chetu naomba niwe muwazi.”
Akizungumza na Mwanaspoti kutoka Mwanza anakouguza majeraha ya nyama za paja, Ngassa alisema amepokea taarifa za kuondoka kwa Kavumbagu na Domayo kwa masikitiko na kuongeza wachezaji hao walikuwa wakihitajika katika kikosi chao.
Ngassa alisema maumivu zaidi yanakuja kutokana na ukweli kwamba wachezaji wote walikuwa katika kikosi cha kwanza cha Yanga, ambapo sasa uongozi unatakiwa kutuliza akili kutafuta mbadala wa nyota hao walioondoka wakiwa wachezaji huru baada ya kumaliza mikataba.
“Tuseme kweli kwamba kuondoka kwa Didier na Domayo ni pengo kwa timu, hili lipo wazi kwani walikuwa wachezaji muhimu katika timu yetu, walicheza mechi nyingi ambazo ni muhimu, ni wakati wa viongozi kufanya kazi yao ipasavyo kuhakikisha wanatafuta wachezaji wengine mahiri ili kuziba nafasi zao,”alisema Ngassa ambaye amewahi kucheza Azam na Simba
Related Posts:
Simba yasajili golikipa mahiri kutoka Zanzibar. Kipa wa JKU ya Zanzibar, Mohammed Abraham Mohammed (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ofisini kwake, Mbezi, Dar es Salaam mara baada ya kusaini Mkataba wa miaka miwili kuit… Read More
TETESI ZOTE ZA USAJILI WA WACHEZAJI BARANI ULAYA. Mchezaji Paul Pogba anawindwa na klabu kubwa barani ulaya zikiwamo Manchester united ,Real Madrid, Manchester City, Chelsea na PSG. Wakala wake Mino Raiola amesema anapokea simu nyingi za ofa ya mteja wake kiung… Read More
Mussa Hassan Mgosi arejea Msimbazi.SIMBA SC imemsajili tena mshambuiaji wake wa zamani, Mussa Hassan Mgosi(pichani)leo hii, baada ya takriban misimu miwili mizuri akiwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Pop… Read More
Falcao kujiunga Mabingwa Chelsea.Radamel Falcao anataraji kujiunga na Chelsea baada ya ndoto zake kwenda vibaya Manchester United. Timu ya Chelsea imeonyesha nia ya kumsaini Radamel Falcao kuwa msaidizi wa Diego Costa. Mcheza huyo miaka 29 anaamini atarudi k… Read More
Nacho Monreal akataa kuongeza mkataba Arsenal.Nacho Monreal amekataa kuongeza mkataba Arsenal kwa mwaka mmoja mbele kutoka mkataba wake wa sasa. Inasemekana anataka kurejea Spain, gazeti la Spanish newspaper AS limeandika. Beki huyo wa pembeni ambaye pia ameshatumika … Read More
0 comments:
Post a Comment