Friday, 16 May 2014
Wizara ya Maliasili Inaongozwa kwa Ubabaishaji
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imesema Wizara ya Maliasili na Utalii inaongozwa kwa ubabaishaji na ‘mvutano wa kimasilahi’ baina ya waziri na katibu mkuu, hivyo kukwamisha shughuli za kuendeleza utalii.
Msemaji wa kambi hiyo (Maliasili na Utalii), Mchungaji Peter Msigwa alitoa kauli hiyo juzi wakati akisoma maoni kuhusu hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa wizara hiyo kwa mwaka 2014/15.
Alisema kambi ya upinzani inasikitishwa na mvutano baina ya Waziri Lazaro Nyalandu na Katibu Mkuu wake, Maimuna Tarishi ambao unaonyesha udhaifu wa Serikali.
“Hii inathibitisha kuwa Serikali ni dhaifu kwa kuwa, waziri na katibu mkuu wa wizara moja wanafanya kazi bila kushirikiana na kila mmoja anaonekana kumvizia mwenzake hadharani badala ya kukaa kwa pamoja kutekeleza maazimio ya Bunge,” alisema Msigwa.
Alisema kitendo cha Waziri Nyalandu kuwasimamisha kazi wakurugenzi wawili, lakini wakarudishwa na katibu mkuu huku akisema taratibu za kuwafukuza hazikufuatwa na hii ni dalili kuwa hata yeye (Nyalandu) siyo msafi kwa kuwa anashindwa hata kujua mipaka yake ya kazi.
Mbali na mvutano huo, Msigwa alisema maazimio ya Bunge kuhusu matokeo ya Operesheni Tokomeza Ujangili yanaendelea kupuuzwa na watumishi wenye tuhuma wakihamishwa vitengo.
“Ngoma ikivuma sana hupasuka, tena Mungu siku zote hamfichi mnafiki na debe tupu haliachi kutika (siyo maneno yangu, bali ya wahenga). Siyo mara ya kwanza kambi ya upinzani kuhoji juu ya usafi wa Lazaro Nyalandu,” alisema.
Related Posts:
Sakata la Mawaziri Mizigo Laibuka Tena.... SAKATA la mawaziri kutajwa kuwa ni mizigo, lililoibuliwa kwa mara ya kwanza na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, limeibuka tena mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha v… Read More
Inatisha:Kikongwe Auwawa kwa Imani za Kishirikina Mauaji ya kutisha yamezidi kuitikisa kahama baada ya Bi Tabu Mtema, miaka 33 mkazi wa kijiji cha BUSULWANGILI Kahama Shinyanga kuuawa kwa kukatwakatwa mapanga na watu wasiojulikana baada ya watu hao… Read More
Lugola:Serikali ya CCM inaendeshwa kisanii Mbunge machachari wa Mwibara, Alphaxard Kangi Lugola, amedai kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo yeye ni mbunge wake, inaendeshwa kisanii.Lugola ambaye katika Bunge lililopita aliwaongoza wabunge wenzak… Read More
Lissu Azidi kufichua maovu:Serekali Itueleze Kwanini Waasisi Sita wa Muungano Waliuwawa na Kuzikwa Kaburi Moja Serikali imetakiwa kutoa maelezo bungeni, kuhusu sababu za kuuawa kwa waasisi sita wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wanaodaiwa kuzikwa katika handaki moja Zanzibar. Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya … Read More
Daktari Afia Gesti DSM MTU mmoja aliyedaiwa kuwa ni daktari wa jijini Mwanza, Raymond Simion (36) amekutwa amekufa ndani ya chumba kwenye nyumba ya kulala wageni ‘gesti’ ijulikanayo kwa jina la Nesta iliyopo Ubungo NHC wilayani Kinondoni ji… Read More
0 comments:
Post a Comment