Wanajeshi wa Boko Haram wanaofanya mashambulizi na kuua raia wasio na 
hatia huko Nigeria wamedaiwa kuanza kukimbia msitu baada ya nyoka wenye
 sumu kali na nyuki kuwashambulia.
Habari hizi zilielezwa na mtuhumiwa mmoja aliyekamatwa na kuthibitisha 
kuwa ni mmoja wa member wa kundi la Boko Haram na alieleza kuwa hivi 
sasa kundi hilo limelazimika kuhama msitu na linaelekea maeneo ya mpaka 
wa Nigeria na Cameroon baada ya wanajeshi wake wa ngazi za juu 
kushambuliwa na nyoka na kupoteza maisha.
Jeshi la Nigeria limeshafanya juhudi za kuwaondoa msituni lakini 
imeshindikana  na hadi sasa kundi hilo linawashikilia wasichana zaidi ya 260
 na bado linaendelea kushambulia Nigeria kwa mabomu ya kutegwa.


0 comments:
Post a Comment