Facebook

Friday 27 June 2014

Jifunze jinsi gani ya ku-Copy/Move ma-file ya Android kama vile ya Whatsapp kutoka kwenye Bluestacks kwenda kwenye Computer


 
Mambo niaje wadau, natumai mabo yanaenda sawa.Leo nilipenda tujifunze kitu muhimu sana wadau, Namna ya kutoa Files zako ulizotumiwa na watu kutoka whatsapp (kwa BLUESTACKS-Android Emulator) ili uziingize kwenye Computer yako wakati mwingine uziamishe zaidi, ubakize kumbu kumbu ama Computer Opertaing system imeleta tatizo....

Wengi Tumekuwa tukikwama sana hapo,halafu unakuta wakati mwingine una data muhimu sana {DATA SENSITIVE} kweli kweli, zingine picha za muhimu sana kumbukumbu na matukio adimu....Basi leo tuiweke sawa kama hivi mdau.


Somo hili la leo linahitaji umakini wa hali ya juu kidogo wadau, Kwa wanaotumia Bluestacks basi cha kwanza kabisa inabidi udownload application ya file manager kwa ajili ya android Mobile OS. (ipo chini kabisa utadownload) Hii app inaitwa
ASTRO File Manager inafanana kama hivi.



Baada ya kudownload Install kwenye Bluestacks yako na baada ya hapo...sasa itakuambia {Prompt} ufanye setup kwa akaunt zako muhimu fanya kwa google account peke yake...nyingine sio muhimu.



Unaweza kuiipata hiyo app hata kwa playstore ya google kama inavyoonekana hapo juu
:whistle: :whistle: :whistle:


Na baada ya KuiNSTALL, Open utakutana na Folder
MNT Fungua utakutana >>>SDCARD

KINACHOFUATA
Sasa mpaka hapo mdau utaweza kukuta kila folder ambalo umekuwa ukishare na wadau mbali mbali vitu vyako kwenye whatsapp, viber, insta na kwingineko.....



Namna ya kuCOPY unafanya ku HOLD ile Folder ama Files ambayo/ambazo ungependa uCOPY data zake....alafu kwa chini utaona OPTIONS za COPY/MOVE ama Delete


UkishaHOLD ukaCOPY basi tunaRUDI kwenye ile path ya
SDCARD baada ya hapo unaenda kwenye folder ya BSTFOLDER Ambapo ndani yake utakuta Folder ya "BSTSHAREDFOLDER" Basi Click hiyo Folder alafu Ingia humo PASTE kile tulichoCOPY kule Mwanzo


Hapa unakuwa kama unazidownload ivi utaona zinaload baadhi ya MB's ama KB's au hata GB's kutokana na wingi wa data zako


SASA KWENYE COMPUTER YANGU NAZIONAJE ??


Usipanic, zipo kwa computer yako kama umefanya kama nlivyo ainisha fresh hapo
:whistle: :whistle: :whistle:

Ili uweze kuziona kwenye computer yako Nenda kwenye Drive C:> (ndio disk ambayo wengi tumekuwa tukifanyia Installations) sasa kachek
>>>ProgramData - BlueStacks - UserData - SharedFolder.

Ebu baada ya Hapo katazame
:dry: :dry: kweeliii ama si kweli???? Afu nambie kama umekwama :silly: basi wapi ulipokwama??? Kama Umefanikiwa :woohoo: :woohoo: :woohoo: THANK YOU. 
 
 

0 comments:

Post a Comment