Facebook

Thursday, 26 June 2014

Ghana yawatimua Muntari na Boateng


Wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa ya Ghana Sulley Muntari na Kevin Prince Boateng wamefukuzwa katika timu hiyo kwa ukosefu wa nidhamu.
Taarifa kutoka mtandao wa shirikisho la soka nchini humo imesema kuwa wawili hao wametimuliwa mara moja.
Boateng anayechezea kilabu ya Schalke 04 amefukuzwa kwa kutoa matamshi machafu yaliomlenga mkufunzi wa timu hiyo Kwesi Appiah wakati timu hiyo ilipokuwa katika mazoezi katika eneo la Maceio.
Naye mchezaji wa AC Milan Sulley Muntari ameadhibiwa kwa kumshambulia afisa mmoja wa kamati kuu ya timu hiyo
Shirikisho la soka nchini Ghana limeongezea kwamba kisa kinachomuhusu Muntari kilitokea siku ya jumanne na kumtaja Moses Armah,mwanachama wa usimamizi wa timu hiyo kama mtu aliyeshambuliwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29.
Wakati huohuo Boateng amedaiwa kutojali matamshi aliyoyatoa.Habari hizo zinajiri siku moja baada ya serikali ya Ghana kutuma dola millioni 3 nchini Brazil ili kuwalipa wachezaji wa timu hiyo nchini Brazil fedha zao za kushiriki katika michuano ya kombe la dunia.
Timu hiyo inayojulikana kama Black Stars ilikuwa imetishia kususia mechi kati yake na Ureno iwapo haitapewa fedha hizo swala lililoilazimu serikali kuingilia kati.

Related Posts:

  • HUU NDIO UZI MPYA WA LIVERPOOL FCRaheem Sterling ambaye wiki iliyopita alikataa mkataba wa kulipwa mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki Liverpool- anaonekana hapa na wachezaji wenzake Martin Skirtel, Simon Mignolet na Daniel Sturridge, wakionesha jezi mpya wat… Read More
  • IFAHAMU HISTORIA YA KLABU YA ARSENAL FC.Mwanzo hadi Vita ya Kwanza ya Dunia Maisha ya klabu ya soka ya Arsenal yalianza pale kikundi cha wafanyakazi katika kiwanda cha kuzalisha zana za kivita cha Woolwich walipoamua kuunda klabu ya soka mwishoni mwa mwaka 1886. Kl… Read More
  • COPA ITALIA : JUVE WAINYUKA FIORENTINA 3-0, HAO FAINALI !!Wakicheza Ugenini bila ya Nyota wao bora, Andrea Pirlo , Paul Pogba na Carlos Tevez, Juventus , chini ya Kocha Massimiliano Allegri, Usiku huu wameipindua kipigo cha mechi ya kwanza na kuichapa Fiorentina 3-0 na kutinga Faina… Read More
  • Ronaldo afutiwa kadi ya njano kwa kosa la kujiangusha.Cristiano Ronaldo sasa ataweza kuichezea Real Madrid vs Elbar wikiendi hii, baada ya kadi ya njano aliyoonyeshwa kwa kosa la kujirusha kufutwa … Read More
  • IBRAHIMOVIC AFUNGIWA MECHI NNEMshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic amefungiwa kucheza mechi nne za ligi kuu ya Ufaransa baada ya kunaswa na picha za televisheni akitukana. Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Sweden alikasirika na kuwashut… Read More

0 comments:

Post a Comment