Kocha wa Uholanzi  Louis van 
Gaal anatarajia shirikisho la soka duniani FIFA  litawaruhusu wachezaji 
wake kunywa maji katika mechi yao ya raundi ya pili dhidi ya Mexico 
itakayochezwa  katika uwanja wa Castelao ulioko katika eneo la  
Fortaleza.
Fortaleza ni eneo linaloshuhudia viwango vya juu vya nyuzi joto.Ni dhahiri kuwa mwili wa binadamu yeyote unastahili maji kwa hivyo hawa wachezaji naamini kuwa wanastahili kunywa maji ilikuzuia wasishikwe na kisunzi .
Van Gaal kiwango cha joto ni juu mno 
Kiungo wao Leroy Fer, ambaye anauguza jeraha la goti anasema kuwa Uholanzi ilipata kionjo tu cha kucheza katika hali ya kiwango cha juu mno cha joto baada ya kuwasili huko wakitoka Rio de Janeiro.
Fer anasema kuwa japo Uholanzi imezoea kucheza katika maeneo ya Uropa yenye baridi kali,Uholanzi itajikaza kisabuni kwani ni hali ileile itakayoikumba timu pinzani ya Mexico.
0 comments:
Post a Comment