![Photo: Tetesi za soka Ulaya
Barcelona hawamtaki tena beki wa Porto Eliaquim Mangala, lakini Chelsea na Manchester United bado wanamfuatilia (Daily Star), Manchester United wapo tayari kutoa pauni milioni 6 kusajili kiungo wa AC Milan Nigel de Jong (Tuttosport), Carlos Vela hatorejea Arsenal na amesaini mkataba mpya Real Sociedad (Daily Express), Tottenham wanajiandaa kutoa pauni milioni 5 kumsajili Divock Origi mwenye asili ya Kenya anayechezea Lille ya Ufaransa (Daily Mail), West Brom wanajipanga kumnyatia Victor Moses wa Chelsea baada ya kushindwa kuonesha cheche zake Liverpool (Sun), Barcelona wameweka dau la pauni milioni 68 kumsajili Luis Suarez kutoka Liverpool (Bild) Manchester United na Tottenham wanamgombea Memphis Depay au "Cristiano Ronaldo mpya" anayechezea PSV Eindhoven (Bild), straika wa Monaco Radamel Falcao amekataa kwenda, Chelsea, Manchester City na Tottenham na anataka kwenda Real Madrid (AS), Real Madrid wapo tayari kuwauza Angel Di Maria, Sami Khedira na Fabio Coentrao iwapo timu zitatoa bei nzuri (Marca). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.](https://scontent-a.xx.fbcdn.net/hphotos-xpf1/t1.0-9/s526x296/10386756_451694388301362_2575431812883960573_n.jpg)
Tetesi za soka Ulaya
Barcelona hawamtaki tena beki wa Porto Eliaquim Mangala, lakini Chelsea na Manchester United bado wanamfuatilia (Daily Star),
Barcelona hawamtaki tena beki wa Porto Eliaquim Mangala, lakini Chelsea na Manchester United bado wanamfuatilia (Daily Star),
Manchester United
wapo tayari kutoa pauni milioni 6 kumsajili kiungo wa AC Milan Nigel de
Jong (Tuttosport),
Carlos Vela hatorejea
Arsenal na amesaini mkataba mpya Real Sociedad (Daily Express),
Tottenham wanajiandaa kutoa pauni milioni 5 kumsajili Divock Origi
mwenye asili ya Kenya anayechezea Lille ya Ufaransa (Daily Mail),
West
Brom wanajipanga kumnyatia Victor Moses wa Chelsea baada ya kushindwa
kuonesha cheche zake Liverpool (Sun),
Barcelona wameweka dau la pauni
milioni 68 kumsajili Luis Suarez kutoka Liverpool (Bild)
Manchester
United na Tottenham wanamgombea Memphis Depay au "Cristiano Ronaldo
mpya" anayechezea PSV Eindhoven (Bild),
Straika wa Monaco Radamel Falcao
amekataa kwenda, Chelsea, Manchester City na Tottenham na anataka
kwenda Real Madrid (AS),
Real Madrid wapo tayari kuwauza Angel Di Maria,
Sami Khedira na Fabio Coentrao iwapo timu zitatoa bei nzuri (Marca).
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.
0 comments:
Post a Comment