Facebook

Monday 23 June 2014

Kumbe watu wengi waliuwawa Nigeria Jumamosi.


Waumini kanisani wakiomba wasichana wa Chibok waachiliwe huru
Inafikiriwa kuwa watu kadha waliuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na wale wanaoshukiwa kuwa wapiganaji Waislamu kaskazini mwa Nigeria hapo jana.
Wakaazi wa huko wanasema wapiganaji wa Boko Haram walikuwapo kwa saa sita, wakiuwa watu na kuchoma moto vijiji.
Inasemekana kati ya waliouwawa ni askari wa usalama.
Baadae wanajeshi na ndege zilipelekwa katika eneo hilo na mtu mmoja aliyeshuhudia tukio hilo, anasema maiti za wapiganaji kadha zimekutikana nje ya vijiji.
Mashambulio hayo yalifanywa karibu na Chibok ambako wapiganaji waliwateka wasichana wa shule zaidi ya 200 mwezi Aprili.

0 comments:

Post a Comment