Suarez
akishika meno yake kuangalia yapo auyametoka baada ya kumng’ata mlinzi
wa Italia Giorgio Chiellini wakati Uruguay ilipokuwa inamenyana na
Italia kwenye mashindano ya Kombe la Dunia 2014, Brazil.
“Nani alimfanya Suarez auwe?,” Maradona aliyasema hayo wakati wa kipindi cha kutoa maoni cha Venezuela Telesur na televisheni ya serikali ya Argentina siku ya Alhamisi usiku.
“Hili ni soka, huu ni mkataba,”alisema gwiji huyo wa Argentina. “Wangeweza hata kumtia pingu na kumpeleka Guantanamo moja kwa moja.”
Guantanamo ni gereza lenye utata la Marekani lililopo nchini Cuba, lilifunguliwa wakati wa utawala wa Bush, linakosolewa zaidi na makundi ya haki za binadamu kwa kuwafunga watu kwa vipindi visivyojulikana bila mashtaka wala kesi.
0 comments:
Post a Comment