Facebook

Friday, 27 June 2014

Kenyatta aongoza kwa umaarufu utumiaji wa Twitter Afrika

Rais Kenyatta amempiku Paul Kagame wa Rwanda kwa idadi ya wafuasi kwenye Twitter
Rais wa Kenya uhuru Kenyatta ndiye Rais anayejishughulisha zaidi kwenye mtandao wa Twitter barani Afrika.
Kenyatta amempiku Rais wa Rwanda Paul Kagame na mwenzake wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Kenyatta ambaye amekuwa mamlakani tu kwa mwaka mmoja, amejipatia wafuasi 456,209, yuko mbele ya mwenzake wa Rwanda Paul Kagame mwenye wafuasi 408,353 ambaye amekuwa mamlakani tangu mwaka 2000, miaka sita kabla hata ya Twitter kuanzishwa.
Rais wa Afrika Kusini anayesifika kwa kashfa mbali mbali, Jacob Zuma ana wafuasi 325,896 akishikilia nafasi ya tatu.
Hata hivyo swali ni je maerais hawa hutumia vipi Twitter? Je wao huwa na mazungumzo ya moja kwa moja na wafuasi wao?
Waziri mkuu wa Uganda, Amama Mbabazi '@AmamaMbabazi,' ndiye kiongozi mwenye kuwasiliana zaidi na wafuasi wake duniani kwenye Twitter huku akiwajibu maswali yao kwake.
408,353, idadi ya wafuasi wa Rais Kagame kwenye Twitter
Asilimia tisini na tano ya mawasiliano yake kwenye Twitter ni '@replies,' ishara ya kuwajibu wafuasi wake. Utafiti huu ni kwa mujibu wa utafiti wa kimataifa kuhusu viongozi wanavyojishughulisha na Twitter, wenye mada, Twiplomacy.
Waziri mkuu mpya wa India, Narendra Modi ana wafuasi milioni 4,967,847 , na anaelekea kushinda Ikulu ya white House ambayo ina wafuasi milioni 4,976,734 katika nafasi ya tano.
Zaidi ya asilimia 83 ya mataifa yote duniani yana uwakilishi katika Twitter, na asilimia 68 ya viongozi wana akaunti za twitter kwa mujibu wa utafiti wa shirika la Burson-Marsteller, nchini Marekani.
Viongozi wanaofuatwa sana kwenye Tiwtter ni pamoja na Barack Obama (@BarackObama) akiwa na wafuasi milioni 43, Papa Francis (@Pontifex) ana wafuasi milioni 14 akifuatiwa na Rais wa Indonesia Susilo Bambang Yudhoyono (@SBYudhoyono) akiwa na wafuasi milioni tano.
Jacob Zuma kama rais anashikilia nafasi ya tatu kwa idadi kubwa ya wafuasi wa Twitter Afrika
Rais Barack Obama alikuwa kiongozi wa kwanza kuanzisha akaunti ya Twitter mwaka 2007.
Kati ya serikali 643 zenye akaunti za Twitter ambazo zilitathminiwa katika nchi 161, ni mataifa 32 pekee hasa yaliyo Afrika na Asia ya Pacific ambayo hayana shughuli nyingi kwenye Twitter.
Utafiti huo pia ulifichua kuwa mawaziri wa mataifa ya kigeni hutumia sana Twitter kutafuta ushirikiano wa kidiplomasia.

Related Posts:

  • Watoto wa ajabu wazaliwa India.Watoto mapacha wa kiume wamezaliwa huko India wakiwa na vichwa viwili katika mwili mmoja kitu ambacho inasemekana ni nadra sana kutokea. Madaktari wamesema wanaamini wanauwezo wa kuokoa maisha ya watoto hao ambao wamezaliwa J… Read More
  • Africa kusini yafunga Mipaka yake ikihofia Ebola. Kila mtu kwao kwa usalama wetu sote. Nchi ya Africa Kusini inafunga mipaka yake kwa wasafiri kutoka katika nchi za Liberia,Guine na Sierra Leone nchi hizo tatu zimeathiriwa vibaya na mripuko wa ugonjwa wa Ebola Waz… Read More
  • Kuku aishi bila kichwa;wengi wapigwa bumbuwazi !  Wakazi wa Kware wakimwangalia jogoo asiye na kichwa ila anatembea!  Wakazi wa eneo la Kware huko Ongata Rongai nchini Kenya wako kwenye mshangao mkubwa kwa kioja ambacho wengi mnaweza msiamini kusikia. Maajabu ha… Read More
  • Hatimaye dawa ya Ebola yapatikana. Tabasamu la matumaini baada ya kupata ahueni ya Ebola Hospitali moja nchini Marekani imewaruhusu wamisionary wawili wa kimarekani ambao walikua wakipata … Read More
  • Boko Haram Wateka Chuo Cha Polisi Nigeria. Boko Haram wazidi kumlaza macho Raisi Jonathan Moyo Kundi la wapiganaji la kiislam la Boko Haram,wamevamia shule moja ya mafunzo ya kipolisi. kituo hicho cha mafunzo kilichoko kwenye kitongoji cha Gwoza kiko karibu… Read More

0 comments:

Post a Comment