Facebook

Friday 27 June 2014

Mkereketwa apigwa risasi na kuuawa Libya

Mzee akisaidiwa kupiga kura nchini Libya katika uchaguzi uliodhaniwa ungeimarisha usalama.
Wakili mashuhuri ambaye pia ni mkereketwa wa haki za kibinadamu nchini Libya ameuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika mji wa Benghazi nchini Libya jana, Jumatano.
Mauaji hayo yametokea baada ya uchaguzi wa Wabunge - ambao wengi walidhani utapunguza visa vya utovu wa usalama.
Wakili huyo mwanamke, anayejulikana sana kwa kupigania haki za wanawake na uhuru wa kisiasa alionekana mara ya mwisho akipiga kura jana.
Salwa Bughaighis alishambulia nyumbani kwake jana jioni.
Ripoti kutoka Benghazi zinasema alishambuliwa na watu waliokuwa na bunduki waliokuwa wamefunika nyuso zao.
Matabibu kutoka hospitali ya Benghazi alikokufia walithibitisha kuwa alikufa kutokana na majeraha ya risasi aliyokuwa nayo kichwani.
Jamaa wake walisema kuwa majirani walimpeleka hospitalini na tangu wakati huo mumewe hajulikani aliko.
Jamii zake wanaamini ametekwa nyara ingawa haijulikani kwa hakika alivyotoweka.
Watu wengi waliosikia habari za kufa wakili huyo wameeleza masikitiko na hasira zao kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Alikuwa miongoni mwa mawakili wa kwanza na mkereketwa aliyepinga kutiwa mbaroni mara kwa mara kwa waandamanaji waliokuwa wakimpinga aliyekuwa mtawala wa Libya, Muamar Gadhafi.

0 comments:

Post a Comment