Facebook

Tuesday 24 June 2014

Dude afiwa na mama yake mzazi!


Kulwa Kikumba (Dude) afiwa na mama yake mzazi! Amefariki leo asubuhi.Soma hapa.
Mwigizaji Kulwa Kikumba maafuru kama (Dude), msanii wa bongo movies,amepata pigo kubwa baada ya kufiwa na mama yake mzazi asubuhi ya leo jijini Dar es salaam taarifa zimetufikia.
 Katika ujumbe wake ambao ameutuma kwa wadau wake, msanii huyo ameandika
“Ndugu zangu wapendwa, nimefiwa na mamaangu mzazi niliyempenda kuliko mtu yeyote kwenye dunia hii, leo . Inna Lillah waa inna illah rajiun”
Taratibu za mazishi zinafanywa na familia ya Marehemu na tutaendelea kwajulisha hapa hapa utaratibu wa mazishi.
Mungu ampe nguvu ya kuweza kusimama imara katika wakati huu mgumu kwake na familia yake kwa ujumla
(Pichani ni msanii huyo akiwa kwenye gari akimpeleka mama yake hospitalini kwa matibabu, kumbe mama huyu tayari alishakuwa ameiaga dunia)
Pole sana kaka Dude!

0 comments:

Post a Comment